logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Malala kuwania ugavana Kakamega baada ya kuponea shoka la mahakama

Jaji wa mahakama ya Kakamega Paul Otieno alisema USIU walitoa dhibitisho ya uhalali wa digrii ya seneta huyo.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku15 July 2022 - 13:04

Muhtasari


• Malaal sasa atamenyana nac Ferdinand Barasa, Cyrusc Jirongo, Samwel Omikoka miongoni mwa wengine.

Seneta Cleopas Malala akihutubia wakazi wa Kakamega

Afueni kwa seneta wa kaunti ya Kakamega Cleophas Malala pamoja na wafuasi wake baada ya mahakama ya Kakamega kutupilia mbali kesi mbili tofauti zilizokuwa zimewasilishwa na wakaazi wawili wa Kakamega wakidai kwamba shahada ya masomo ya seneta huyo sio halali.

Akitoa uamuzi huo jaji wa mahakama ya Kakamega  Paul Otieno amesema walalamishi hawakuwa na ushahidi wa kutosha kudhihirisha kuwa stakabadhi za Malala ni ghushi.

Wakaazi hao wawili Fred Muka na Frankline Shilingi waliwasilisha kesi hizo wakiitaka mahakama isimruhusu Malala kuwania  ugavana wakidai kwamba kuna utata kuhusu vyeti vyake vya masomo.

Jaji Otieno pia alisema chuo cha USIU kilitoa ushahidi mbele ya mahakama hiyo kwamba seneta Malala alisoma na kuhitimu na shahada ya Mawasiliano na Utandawazi kutoka chuo hicho kilichopo viungani mwa mji wa Nairobi.

Sasa seneta huyo aliyechaguliwa kwa tikiti ya chama cha ANC ako huru kuendelea na azma yake ya kuwa mrithi wa gavana Oparanya kupitia tikiti ya chama cha UDA.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved