logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kajala aingilia kati talaka ya Harmonize, Sarah adaiwa kutaka wagawane mali

Harmonize anakusudia kuandika talaka tatu baada ya mwanamitindo huyo kumshtaki.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 September 2022 - 08:08

Muhtasari


•Kwa sasa Sarah yupo nchini Tanzania kwa ajili ya muendeleo wa talaka yake na Harmonize, takriban miaka miwili baada yao kutengana.

Bosi huyo wa Kondegang ameshauriwa na mchumba wake Kajala asifadhaishwe na mpenziwe huyo wa zamani.

Drama zimeendelea kutanda kati ya staa wa Bongo, Harmonize na aliyekuwa mpenzi wake wa muda mrefu Sarah Michelloti.

Kwa sasa Sarah yupo nchini Tanzania kwa ajili ya muendeleo wa talaka yake na Harmonize, takriban miaka miwili baada yao kutengana.

Imeibuka kuwa sasa Harmonize anapanga kuandika talaka tatu baada ya mwenzi huyo wake wa zamani kuwasilisha kesi mahakamani.

"Yani anashtaki kama mimi nimemuoa!"  Harmonize alimuandikia mchumba wake wa sasa muigizaji Kajala Masanja kwenye screenshot ya mazungumzo yao aliyochapisha kwenye Instastori zake.

Katika mazungumzo hayo, aliendelea kufichua kuwa sababu ya Sarah kudai talaka ni kwa kuwa anataka wagawane mali.

Hata hivyo alidokeza kuwa hakuna mali yoyote ambayo anapaswa kugawana na mwanamitindo huyo kutoka Italia huku akibainisha kuwa aliondoka bila chochote wakati walipoachana mwishoni mwa mwaka 2020.

"Tumeachana nikaanza kulala nyumbani kwako daah hata pa kulala nilikuwa sina. Hizo mali zilikuwa wapi jamani!! Daah," alimwandikia Kajala.

Bosi huyo wa Kondegang hata hivyo ameshauriwa na mchumba wake Kajala asifadhaishwe na mpenziwe huyo wa zamani.

"Achana naye," alimshauri.

Harmonize ambaye alionekana kufurahishwa na ushauri wa mchumba wake alisema,  "LOL, hata mke wangu hasumbuki. Kuwa na mwanamke mwenye akili haha!! Niko high tu, sijui mbona napost!"

Jumatano Bi Sarah  alifika katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke huko Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya talaka yake na Harmonize.

Video iliyofikia Radio Jambo ilimuonyesha mwanamitindo huyo mahakamani akiwa ameandamana na baadhi ya wanafamilia wake

Sarah ambaye alitengana na Harmonize takriban miaka miwili iliyopita aliripotiwa kufika mahakamani kufuatilia madai ya talaka yao. Wawili hao walikuwa kwenye ndoa kwa takriban miaka minne.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved