logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Daktari alisema nimemaliza mayai,'Akothee ajibu madai ya kuwa mjamzito

Akothee alisema kwamba anatamani kuku na wala sio kwa ajili ana mimba.

image
na Radio Jambo

Makala18 November 2022 - 19:30

Muhtasari


  • Alitupilia madai hayo mbali siku ya Ijumaa kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook,hii ni baada ya mashabiki kusema kamba mama huyo wa watoto 5 alikuwa anatarajia mtoto mwingine

Mjasirimali na msanii shupavu nchini Esther Akoth almaarufu Akothee ametupilia mbali madai kwamba ni mjamzito.

Alitupilia madai hayo mbali siku ya Ijumaa kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook,hii ni baada ya mashabiki kusema kamba mama huyo wa watoto 5 alikuwa anatarajia mtoto mwingine.

Akothee alisema kwamba anatamani kuku na wala sio kwa ajili ana mimba.

Pia aliwatania mashabiki wake na kuwataarifu kwamba daktari alimwambia mayai ya uzazi yamekwisha.

Kwa haraka sana mashabiki wake walimtumia Akothee jumbe za pongezi.

"Kuku wa limau ukiwa na chumvi nyingi😭😭😭😭😭ngoja mimi sio mjamzito, ni utoto inanisumbua. Keep the congratulations haki, mimi hata daktari alisema nimemaliza mayai ,labda miracle baby 🙊,"Aliweka wazi Akothee.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved