logo

NOW ON AIR

Listen in Live

MCA Tricky awekwa chini ya shinikizo la kuoa

Mchekeshaji MCA Tricky yuko chini ya shinikizo la kuoa na kupata watoto.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri15 March 2023 - 03:48

Muhtasari


•Katika mahojiano na Word Is, mchekeshaji huyo alisema mama yake hataki kusikia kitu kingine chochote mwaka wa 2023.

•"Lazima niwe na uhakika kabla ya kumtambulisha kwa mama yangu," alisema

Mchekeshaji MCA Tricky yuko chini ya shinikizo la kuoa na kupata watoto.

Katika mahojiano na Word Is, mchekeshaji huyo alisema mama yake hataki kusikia kitu kingine chochote mwaka wa 2023.

Alisema anachumbiana lakini bado hajamtambulisha mpenzi wake kwa mama yake.

"Lazima niwe na uhakika kabla ya kumtambulisha kwa mama yangu," alisema na kuongeza kuwa anapanga kutulia mwaka huu baada ya kutimiza miaka 30.

"Mama yangu ananikasirikia kwa sababu anadhani ninapaswa kuwa na watoto watatu.

"Sitafichua mengi kwa mashabiki wangu, hata baada ya kuweka mambo rasmi.

MCA Tricky anatangaza shoo yake ijayo, 'A Tricky Comedy Circuit', itakayofanyika Nairobi Cinema mnamo Machi 31.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved