logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshtuko baada ya warembo kujitokeza wakidai wana mimba ya mwimbaji Davido

Baada ya Anita kujitokeza, mrembo wa Ufaransa, Ivanna Bay pia alijitokeza kudai kuwa ana ujauzito wa mtoto wa Davido.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 June 2023 - 04:31

Muhtasari


•Anita alifichua gumzo yake na mwimbaji huyo wa Afrobeats kwa madai kuwa amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi naye na hata anatarajia mtoto naye.

•Kupitia mtandaoni, Ivanna alibainisha kuwa hakujua kuwa sio yeye pekee ambaye mwimbaji huyo alitunga ujauzito.

Mwanamke wa pili amejitokeza na kudai kuwa yeye pia ana mimba ya mwimbaji wa Nigeria David Adedeji Adeleke almaarufu Davido katika muda wa siku mbili tu.

Siku ya Jumatano, mrembo wa Marekani, Anita Brown almaarufu Ninatheelite alifichua gumzo yake na mwimbaji huyo wa Afrobeats kwa madai kuwa amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi naye na hata anatarajia mtoto naye.

Anita alidai alikutana na mwimbaji huyo mwaka wa 2017, wakiwa safarini Dubai na wawili hao wakawa kwenye uhusiano wa mbali hadi 2020 wakati janga la Corona lilitokea.

“Kinachoniuwa sana ni simulizi hii ya wanaume waliolewa ambayo nyinyi nyote mnaiburuza, oh najihusisha na mwanamume aliyeoa, acheni, hapana sikujua kuwa ameolewa haki ya Mungu, sikujua kama ameolewa, nenda kwenye ukurasa wake , je inaonekana kama ameoa ama nimechanganyikiwa?,” Anita aliwaambia watu waliokuwa wakimshutumu kwa kuchumbiana na mwanamume aliyeoa.

Katika screenshot za yanayodaiwa kuwa mazungumzo yao ambayo Anita alichapisha, Davido alionekana akimsihi asimwambie mtu yeyote kuwa yeye ndiye baba wa mtoto wake ambaye hajazaliwa.

Pia alidai kuwa Davido alimpa pesa ili kuitoa mimba hiyo, lakini alikataa.

“Sikuwa na hamu ya kuolewa hivi sasa. Niligundua baadaye kwamba mimi ni mjamzito, kwa hivyo mko mbali," Anita alisema.

Saa chache tu baada ya Anita Brown kujitokeza, mwanamke wa Ufaransa, Ivanna Bay alijitokeza pia kudai kuwa ana ujauzito wa mtoto wa Davido.

Kupitia mtandaoni, Ivanna alibainisha kuwa hakujua kuwa sio yeye pekee ambaye mwimbaji huyo alitunga ujauzito.

"Niliamka asubuhi na kuona kwamba sio mimi pekee mwanamke ambaye David alipata ujauzito. Nimesikitishwa sana na mtu wa aina hii. Wanawake, kuweni makini. Bado nina mimba. Kwa hivyo tuonane chini ya miezi 9 sasa,” Ivanna aliandika.

Aliendelea, "Kwa hivyo niambieni, uko na baby mama wangapi, je, tunapaswa kuwa tayari kwa timu ya soka?"


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved