logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lupita Nyong’o ajivinjari na mpenziwe mpya miezi baada ya kumtema Selema Masekela

Lupita na Jackson walihusishwa kimapenzi kwa mara ya kwanza mnamo Oktoba 2023 baada ya wawili hao kutengana na wenzi wao.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku05 March 2024 - 12:53

Muhtasari


•Wawili hao walionekana wakiwa wameshikana mikono kimahaba wakitembea kando ya ufuo wa Puerto Vallarta, Mexico.

•Lupita na Jackson walihusishwa kimapenzi kwa mara ya kwanza mnamo Oktoba 2023 baada ya wawili hao kutengana na wenzi wao. 

Miezi michache tu baada ya kuthibitisha kuvunjika kwa mahusiano yake na mtangazaji wa masuala ya spoti Selema Masekela, mugizaji mashuhuri wa Kenya na Canada Lupita Nyong'o anaonekana kujitosa kwenye dimbwi la mahaba na muigizaji mwenzake Joshua Jackson kutoka Canada.

Ripoti za uhusiano wa wawili hao zimekithiri katika muda wa saa chache zilizopita baada ya picha nzuri za waigizaji hao kuibuka kwenye mitandao ya kijamii.

Picha ambazo zilionekana na Radio Jambo zinamuonyesha Lupita na mzungu huyo mwenye umri wa miaka 45 wakiwa wameshikana mikono kimahaba wakitembea kando ya ufuo wa Puerto Vallarta, Mexico ambapo binti huyo wa gavana Anyang’ Nyong’o alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ya 41. Wawili hao wote walikuwa wamevalia mavazi mepesi ya kuogelea.

Waigizaji hao mashuhuri pia walionekana wakikimbia baharini pamoja na pia karibu wakibusiana katika picha zinazosambazwa sana kwenye mitandao ya kijamii.

Lupita na Jackson walihusishwa kimapenzi kwa mara ya kwanza mnamo Oktoba 2023 baada ya wawili hao kutengana na wenzi wao. Joshua aliachana na mkewe Jodie Turner-Smith na Nyong'o akatengana na aliyekuwa mpenzi wake kutoka Selema Masekela.

Lupita Nyong’o alimaliza uhusiano wake na mpenzi wake Selema Masekela mnamo Oktoba 2023 baada ya kuchumbiana kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Lupita ambaye alionekana kuhuzunika alitoa tangazo la kutengana na Masekela kupitia mitandao yake ya kijamii akisema "ni muhimu kwangu kushiriki ukweli wa kibinafsi na kujitenga hadharani na mtu ambaye siwezi kumwamini tena,".

Wapenzi hao wa zamani walitengana takriban mwaka mmoja baada ya kuweka hadharani uhusiano wao.

Lupita alitangaza kutengana kupitia mtandao wake wa kijamii mnamo Oktoba 19, 2023. Wawili hao walitangaza uhusiano wao hadharani mnamo Desemba 2022.

Wakati huo, mwigizaji wa Black Panther alitumia mitandao yake ya kijamii kumpigia debe Selema Masekela - kama ufichuzi kuwa wako kwenye uhusiano wa kimapenzi.

Lupita alikuwa akichumbiana na Selema Masekela mwenye umri wa miaka 51 akiwa na miaka 39.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved