logo

NOW ON AIR

Listen in Live

June Chebet, bintiye Rais wa zamani Moi afariki

Katika tangazo la Alhamisi, familia ilisema Chebet alifariki asubuhi.

image
na

Habari11 April 2024 - 06:21

Muhtasari


• "Tuna huzuni kubwa kutangaza kifo cha mpendwa wetu, June Chebet Moi asubuhi ya leo," taarifa hiyo ilisema.

JUNE CHEBET

June Chebet, bintiye Rais wa zamani Daniel Arap Moi amefariki dunia.

Katika tangazo la Alhamisi, familia ilisema Chebet alifariki asubuhi.

Familia hata hivyo haijafichua maelezo zaidi kuhusu kifo chake, na kuomba faragha wakati wa maombolezo.

"Tuna huzuni kubwa kutangaza kifo cha mpendwa wetu, June Chebet Moi asubuhi ya leo," taarifa hiyo ilisema.

"Wakati huu wa majonzi, tunaomba dua na faragha yako wakati sisi familia tukipokea msiba wa dada yetu. Roho yake ipumzike kwa amani ya milele," iliongeza.

Taarifa zaidi zinafuata...


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved