logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pascal Tokodi adokeza ndoa yake na Grace Ekirapa bado ipo imara

aliposti ujumbe wa kufurahisha wa kuzaliwa akimsherehekea mtangazaji huyo wa zamani wa NTV, akimmwagia sifa tele.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku29 April 2024 - 12:28

Muhtasari


  • Pascal alimjibu shabiki kwa haraka kuweka maelezo ya uhusiano wao kuwa ya faragha na kuwapa mashabiki waliouliza swali hilo ushauri.

Muigizaji mashuhuri wa Kenya Pascal Tokodi amevunja ukimya kuhusu uvumi wa kutengana kwake na mkewe Grace Ekirapa, akiwapuuzilia mbali wakosoaji kumtetea mke wake alipoulizwa kuhusu uvumi wao wa kutengana.

Yote ilianza wakati muigizaji huyo aliposti ujumbe wa kufurahisha wa kusherehekea siku ya kuzaliwa akimsherehekea mtangazaji huyo wa zamani wa NTV, na kummwagia sifa tele.

"Nilijua utakuwa mama wa ajabu Mama AJ na unaendelea kuwa mmoja kila siku, ulinipa zawadi bora zaidi ambayo sijawahi kupata na nitashukuru milele ...., asante Mama ... ...asante kwa kuwa mzazi wa ajabu kwa mtoto wetu 🙌❤️🫂Heri njema ya siku ya kuzaliwa @graceekirapa", ilisoma ujumbe wa Pascal kwa Grace.

Baadhi ya wanamtandao walikuwa wepesi kuhukumu ujumbe ulioandikwa na Pascal wakibainisha kuwa mwigizaji huyo alikuwa akimsherehekea Grace kama mama mzuri kwa binti yao bila kumtaja kama mke, huku mmoja akitafuta ufafanuzi.

Wengine waliuliza kwa nini hakuonyesha upendo wake kwake mara nyingi kama wanandoa wengi wanavyofanya wanapoadhimisha matukio muhimu kama vile siku za kuzaliwa na maadhimisho ya harusi.

Shabiki mmoja alitoa maoni yake; "The wish seems dry man. Did you really break up?"

Mwingine naye alitoa maoni yake, "Ni kweli, hata jina la 'Love' halijatajwa, hii yote ni kuhusu Mama AJ. Birthday wish ni fupi sana. Tuliienzi sana hii ndoa lakini inaonekana hata shetani alikuwa na mkono ndani yake".

Pascal alimjibu shabiki kwa haraka kuweka maelezo ya uhusiano wao kuwa ya faragha na kuwapa mashabiki waliouliza swali hilo ushauri.

"Fagia nyumba yako mwenyewe", Pascal alijibu.

"Grace Ekipara naye alitoa maoni yake kuhusu chapisho la Pascal akisema; "Yaani nahitaji taulo zima la macho yangu, asante kwa matakwa mazuri na asante kwa kunichagua kama mama kwa zawadi hii nzuri tunayependa❤️❤️❤️❤️"


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved