logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wasiwasi huku akaunti ya Twitter ya Maverick Aoko yenye wafuasi wengi ikifungwa

Akaunti ya Aoko ya X yenye wafuasi zaidi ya 330,000 ilionekana kuzimwa siku ya Jumanne jioni .

image
na Samuel Mainajournalist

Dakia-udaku13 November 2024 - 15:09

Muhtasari


  • Haya yanajiri siku chache tu baada ya taarifa ambayo ilidaiwa kutolewa na Aoko mwenyewe kuchapishwa kwenye jukwaa hilo ikibainisha kuwa yuko sawa.
  • Aoko alitoweka kwenye mitandao ya kijamii wiki chache zilizopita.

Wasiwasi mkubwa umeibuliwa haswa kwenye mtandao ya kijamii wa X baada ya akaunti ya mwanahabari maarufu Scophine Aoko almaarufu Maverick Aoko kuzimwa.
Akaunti ya Aoko ya X yenye wafuasi zaidi ya 330,000 ilionekana kuzimwa siku ya Jumanne jioni baada ya kuwepo kwa zaidi ya muongo mmoja. Akaunti hiyo iliundwa mnamo Septemba 2013 na mwanahabari huyo amekuwa akitumia jukwaa hilo kuripoti habari, kuandika blogu za kisiasa, uanaharakati miongoni mwa mambo mengine.

Kufikia wakati wa kuchapishwa kwa makala haya, mtu hangeweza kufikia akaunti ya Aoko (@AokoOtieno_,) kwani hitilafu ilitokea wakati wa kujaribu kufanya hivyo.

“Neno ulioingiza halikuleta matokeo yoyote. Tafadhali jaribu tena baadaye,” ilisoma arifa iliyotokea wakati wa kujaribu kufikia akaunti.

Hili limezua wasiwasi mwingi miongoni mwa watumiaji wa mtandao, hasa watumiaji wa X huku wengi sasa wakijaribu kuzungumzia na kukisia ni nini kilitokea.

Haya yanajiri siku chache tu baada ya taarifa ambayo ilidaiwa kutolewa na Aoko mwenyewe kuchapishwa kwenye jukwaa hilo ikibainisha kuwa yuko sawa.

Aoko alitoweka kwenye mitandao ya kijamii wiki chache zilizopita na katika siku zilizofuata, wanamtandao wengi walikuwa wakielezea wasiwasi wao kuhusu hali yake na kutaka kujua aliko.

 Siku ya Ijumaa wiki jana, mwanahabari huyo alitoa taarifa ndefu kwenye jukwaa la X akielezea jinsi akaunti yake imekuwa ikisimamiwa wakati wa kutokuwepo kwake na jinsi amekuwa.

 “Mtu ambaye amekuwa akichapisha kwenye akaunti yangu amekuwa na ruhusa isiyohifadhiwa yangu na ya Familia yangu. Kutokuamini kwenu kunakubalika, mashaka hayo ni halali ikizingatiwa kuwa tunakabiliana na utawala mkali usio na mipaka,” Aoko alisema.

 Aliongeza, “Hata hivyo ninawahakikishia; walinipata lakini sio akaunti yangu. Sisi si watu wajinga jinsi wanavyotudhania kuwa na jambo la kwanza ambalo msaidizi wangu hufanya ninapopiga simu kwa dharura, au haipatikani, ni kubadilisha nywila zetu. Hii sio tu inalinda akaunti hii lakini pia vyanzo vyangu kwa maana inapita bila kusema, bila wao, hakuna 'Chai.'

 Pia alithibitisha kuwa Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino alifuatilia na familia yake ili kuthibitisha kuhusu hali yake baada ya kuripotiwa kutoweka.

 Akizungumzia hali lake, alibainisha kuwa yu hai na akashukuru kila mtu ambaye alikuwa ameibua wasiwasi wake juu na kumuombea usalama.

 “Nini kilitokea? Nitawaambia, oh nitafichua kila undani wa dakika, kila chembe ... Lakini tutazungumza marafiki wapendwa zaidi nitakapokuwa bora. Kadiri usiku unavyozidi kuwa giza, ndivyo nyota zinavyong’aa. Nikiwa na kiwewe, nachagua kutopapasa na kugaagaa gizani, wakati naweza kustaajabia kilicho huko huko,” alisema.

 Aoko alitoweka kwenye mitandao ya kijamii mnamo Oktoba 21, jambo lililozua wasiwasi mwingi kwenye mitandao ya kijamii.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved