logo

NOW ON AIR

Listen in Live

MP Salasya kutumia shilingi milioni moja kusherehekea watahiniwa waliopita mtihani wa kidato cha 4

PK Salasya amehongera shule ya upili ya wasichana ya Shitoto na Kamashia zinazopatikana katika eneobunge lake

image
na Brandon Asiema

Dakia-udaku10 January 2025 - 11:52

Muhtasari


  • Sherehe ambayo mbunge huyo anapanga kufanyika mwezi wa tatu itawajumuisha watahiniwa wa mwaka huu.
  • Shule ya Shitoto iliandikisha alama ya wastani ya 7.0 Salasya akiisifia kuwa shule ya mashambani.


Mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya amesema kuwa atalazimika kutafuta shilingi milioni moja ili kuandaa sherehe ya kuwasherehekea wanafunzi waliofanya mtihani wa sekondari mwaka jana kutoka eneobunge lake.

Mbunge huyo ameelezea furaha ya wanafunzi kutoka shule kadhaa katika eneo bunge lake kupata alama bora ambazo zitawawezesha kujiunga na vyuo vikuu nchini.

Kwenye ukurasa wake wa Instagram, PK Salasya amehongera shule ya upili ya wasichana ya Shitoto kwa kuwa na matokeo bora ambapo zaidi ya wanafunzi arubaini wamepata alama za moja kwa moja kujiunga na vyuo vikuu mbali mbali nchini kuendeleza masomo yao katika taaluma na nyanja mbali mbali.

Aidha mbunge huyo amejisifu akidai kuwa tangu kuchaguliwa kama mbunge wa Mumias Mashariki, matokeo ya wanafunzi katika mitihani ya kitaifa imeimarika kutokana na uwekezaji kwa maswala ya elimu na uongozi.

Shule ya Shitoto iliandikisha alama ya wastani ya 7.0 Salasya akiisifia kuwa shule ya mashambani.

“Hii shule kabla sijaingia kwenye uongozi ilikuwa na perfoming vibaya sana lakini nilipoingia kwenye uongozi niliomba mabadiliko makubwa shuleni na kwa support yangu na kwa support yangu madam principal amenipa nilichokuwa nakitaka.”  Aliandika Salasya kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Mbali na shule ya wasichana ya Shitoto, mbunge Salasya pia amesifia shule ya sekondari ya Kamashia ambayo kwenye matokeo yake, wanafunzi 141 wamefuzu moja kwa moja kujiunga na vyuo vikuu. Shule hiyo, iko na alama ya wastani ya 7.565 inayoashiria alama ya B chanya.

Sherehe ambayo mbunge huyo anapanga kufanyika mwezi wa tatu itawajumuisha watahiniwa wa mwaka huu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved