logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize awapa onyo wanaomdhalilisha mchumba wake mpya

Mwanamziki kutokea Tanzania Harmonize ametoa onyo la hatari kwa wale wanamdhalilisha mchumba wake mpya Abby Chams..

image
na Japheth Nyongesa

Dakia-udaku15 January 2025 - 15:53

Muhtasari


  • Harmomize alimhusisha Abby Chams katika wimbo wake wa  “ Closer”, mwaka jana 2024. 
  • Mwanamziki huyo amedinda kuzungumzia kuhusu swala lililomfanya yeye kutengana na mchumba wake wa zamani Poshy Queen

caption


Mwanamziki kutokea Tanzania Harmonize ametoa onyo la hatari kwa wale wanamdhalilisha mchumba wake mpya Abby Chams..

Kwenye ukurasa wake wa instagrm aliwatahatharisha wanablogu pamoja na vyombo vya habari na kuwataka kumuacha mchumba wake kabisa.

Alisema kuwa anampenda sana mwanamke wake na mtu yeyote hafai kumzungumzia visivyo.

“Niko kiukweli kabisa kuhusu hili, sitaki kusikia chochote kuhusu mchumba wangu. Wanablogu na wanahabari msitaje mchumba wangu kwa mambo mabaya yasiyo na heshima, hilo linaniumiza sana,  linapofika masikioni mwangu. Alisema mwana mziki huyo aliyeimba kibao kinachotrend kwa sasa. “ MATATIZO”

Abby Chams ambaye jina lake halisi Abigail Chamungwana pia ni mwanamziki ambaye amefanya collabo na wasani wakubwa tokea Tanzania akiwemo Ali Kiba na boyfriend wake wa sasa Harmonize. 

Wawili hao walianza mahusiano yao muda mchache baada ya harmomize kumuhusisha katika wimbo wake wa  “ Closer”, mwaka jana 2024.

Hao wanamziki walianza mahusino yao rasmi baada ya Harmonize kutangaza hadharani kuachana na mchumba wake wa zamani Poshy Queen Oktoba mwaka jana. Hata hivyo mwanamziki huyo amedinda kuzungumzia kuhusu swala lililomfanya yeye kutengana na mchumba wake huyo wa zamani. Wawili hao walitengana baada ya kuwa kwa mahusiano kwa miaka miwili.

“Niko macho naona kila kitu ambacho kinazungumziwa katika mahusiano yangu mapya. Niaminini sijafurahia. Siwezificha kile ambacho nimekiweka hadharani. Kimya changu ni kwa sababu sitaki watu wazungumze mambo tofauti. Heshima yang kwa famila yao ni kubwa sana na hatujafaulu kuwa pamoja milele. Tunafaa kuelewa kwamba kila kitu hupangwa na mwenyezi Mungu,” Harmonize alielezea hili kuhusu mapenzi yake ya zamani.

Kwa sasa Star huyo wa bongo Tanzania amemteuwa mpenzi wake huyo wa zamani Poshy Queen kama afisa mtendaji [ CEO] wa kampuni yake ya kamari [betting company] inayojulikana kama Bukua Milioni.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved