logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama yaamuru Kinyonga aliyepewa mafunzo kumroga rais kupelekwa ‘rehab’

Kinyonga huyo ni miongoni mwa vitu vingi vya kishirikina vilivyonaswa na washukiwa wawili – waganga wa kienyeji – ambao walikamatwa Desemba 2024 kwa tuhuma za kuroga rais.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Dakia-udaku06 March 2025 - 12:37

Muhtasari


  • Kulingana na afisa huyo wa idara ya wanyamapori, mnyama huyo alipewa mafunzo ya kubadili rangi kwa njia ambayo "itamchanganya na kumdhoofisha" Rais.
  • Kufuatia "kukamatwa" kwake, kinyonga huyo alitumwa rehab kwa ajili ya kurekebisha tabia.

kinyonga

KATIKA kesi isiyo ya kawaida, mahakama ya juu nchini Zambia imetoa uamuzi wa kinyonga anayedaiwa kupatiwa mafunzo ya jinsi ya kumroga rais wa taifa hilo, Hachilema Hakainde kupelekwa katika kituo cha kurekebisha tabia.

Kinyonga huyo ni miongoni mwa vitu vingi vya kishirikina vilivyonaswa na washukiwa wawili – waganga wa kienyeji – ambao walikamatwa Desemba 2024 kwa tuhuma za kuroga rais, jarida la Zambain Observer liliripoti.

Washukiwa hao waawili, Leonard Phiri (43) na Jasten Candunde (42) wanakabiliwa na makosa mawili: Kumiliki hirizi na Kukiri ujuzi wa uchawi.

Akitoa ushahidi wake mbele ya Mahakama ya Lusaka, Ofisa wa Idara ya Wanyamapori ya Lilayi, Bright Nkhoma, aliiambia mahakama kuwa kinyonga huyo ni sehemu ya mkusanyo wa hirizi aina ya juju waliokutwa na watuhumiwa hao.

Lakini ilikuwa jukumu la kinyonga katika njama hiyo iliyodaiwa kuwaacha kila mtu katika chumba cha mahakama akiwa ameshtuka na kufurahishwa.

Kulingana na afisa huyo wa idara ya wanyamapori, mnyama huyo alipewa mafunzo ya kubadili rangi kwa njia ambayo "itamchanganya na kumdhoofisha" Rais.

Kufuatia "kukamatwa" kwake, kinyonga huyo alitumwa rehab kwa ajili ya kurekebisha tabia.

Wakati Phiri na Candunde wakisubiri hatima yao mahakamani, kinyonga huyo sasa anasemekana kuzoea maisha, akipokea "huduma" na pengine kutafakari maisha yake mafupi katika ulimwengu wa siasa na uchawi.

Wakati wa kukamatwa mwaka jana, Msemaji wa polisi, Rae Hamoonga alisema katika taarifa yake kwamba washukiwa hao wawili, wanadaiwa kukodiwa na Nelson Banda, mdogo wa mbunge mtoro Jay Banda, ili kumroga rais.

Jay Banda alitoroka kutoka mikononi mwa polisi Agosti 2024 akikabiliwa na shtaka la wizi wa kupindukia. Mahali alipo hajulikani.

Washukiwa hao wawili wanakabiliwa na mashtaka ya kufanya uchawi, kumiliki hirizi na ukatili kwa wanyama.

Msemaji wa polisi alisema washukiwa hao walifichua kwamba walikubali kupokea malipo kamili ya $7,400.

"Dhamira yao iliyodaiwa ilikuwa kutumia hirizi kudhuru" Rais Hakainde Hichilema, alisema taarifa ya polisi, iliyotolewa Ijumaa.

Kesi hiyo inapoendelea, Watu wanabaki wakiuliza: Nani alijua hata vinyonga wana taaluma katika uchawi?

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved