logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mke aenda kortini kumtaliki mumewe sababu anafanya mapenzi usiku kucha bila kuchoka!

Alisema kwamba amejaribu kuvumilia lakini ameona ni kama anaumia kwani amefika mwisho na katu hawezi kustahimili kiu cha mapenzi cha mumewe.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Dakia-udaku26 March 2025 - 10:20

Muhtasari


  • Stephen, Mumewe katika majibu yake, aliiambia mahakama kuwa anampenda mkewe na bado anamhitaji.
  • Stephen alisema amekuwa akimsihi mke wake asitake talaka, kwani sasa yuko tayari kudhibiti hamu yake ya kujamiiana.
  • "Niliwapeleka wajomba na marafiki nyumbani kwa wazazi wake ili kumsihi. Lakini alikataa kutusikiliza badala yake alituacha," Stephen alisema.

Wanandoa katika mfarakano

MWANAMKE mmoja mwenye umri wa miaka 37 aliishangaza mahakama ya kusuluhisha migogoro ya ndoa baada ya kuwasilisha ombi la talaka kutoka kwa mumewe akidai anampelekea moto mkali.

Kwa mujibu wa Vanguard, mwanamke huyo kutoka jimbo la Kaduna nchini Nigeria alielezea mahakama kwamba amechoka na ndoa yake kwa sababu mumewe anafanya mapenzi naye kila siku usiku kucha bila kuchoka na hampi muda wa kupumzika.

Alisema kwamba amejaribu kuvumilia lakini ameona ni kama anaumia kwani amefika mwisho na katu hawezi kustahimili kiu cha mapenzi cha mumewe.

Katika ombi lake, Bi Linda, pia alimshutumu mumewe kwa kumpiga kila alipokataa matamanio yake ya kufanya mapenzi, jambo ambalo limemfanya kuona ndoa ya miaka 6 kuwa chungu.

Aliambia mahakama kuwa havutiwi tena na ndoa hiyo kwani hawezi tena kustahimili hitaji la kupita kiasi la mumewe.

"Ninaiomba mahakama kuvunja ndoa hii kwa sababu siwezi kustahimili hamu yake ya kujamiiana kupita kiasi. Anapenda mapenzi kupita kiasi, na siwezi kuvumilia.”

"Mara nyingi alikuwa akifanya mapenzi na mimi kuanzia usiku wa manane hadi alfajiri, hata nikilia haachi.”

"Imepita miezi mitatu tangu nihame nyumbani kwake, ndugu zake wamekuwa wakinisihi nirudi kwake, lakini hawajui ninachokabiliana nacho," alisema.

Alisema zaidi kwamba mume wake hajidhibiti wakati wowote anapohitaji mapenzi, na kwamba wakati wowote alipokataa matamanio yake ya kufanya mapenzi, alikuwa akimpiga, hata mbele ya watoto wao wawili.

Stephen, Mumewe katika majibu yake, aliiambia mahakama kuwa anampenda mkewe na bado anamhitaji.

Stephen alisema amekuwa akimsihi mke wake asitake talaka, kwani sasa yuko tayari kudhibiti hamu yake ya kujamiiana.

"Niliwapeleka wajomba na marafiki nyumbani kwa wazazi wake ili kumsihi. Lakini alikataa kutusikiliza badala yake alituacha," Stephen alisema.

Aidha aliiomba mahakama kumpa muda wa kurekebisha mambo na kurudiana na mkewe.

Hakimu aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 6 kwa ajili ya kupata mrejesho na matokeo ya maridhiano hayo huku akiwashauri kudumisha amani.

Ni kesi ambayo imevutia usikivu wa wengi haswa mitandaoni, baadhi wakidai kwamba hamu ya mapenzi ya mume huyo ni ndoto na tamanio la wanawake wengi huku wengine wakidai kwamba huenda alikuwa anatumia dawa za ziada za kuongeza nguvu na hamu yake.

 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved