"Nilikuwa mkubwa zaidi darasani" Pritty Vishy azungumzia kumaliza sekondari 2022

Vishy amesisitiza kwamba alimaliza masomo yake ya shule ya upili takriban miaka miwili iliyopita.

Muhtasari

•Mrembo huyo mwenye umri wa miaka 22 alisema kwamba alifanya mtihani wake wa KCSE mnamo Machi 2022.

•Vishy alizungumza kuhusu  jinsi alivyokuwa mkubwa zaidi katika darasa lao na jinsi mama yake angeweza kumtia moyo 

Image: INSTAGRAM// PRITTY VISHY

Mtayarishaji wa Maudhui mashuhuri wa Kenya, Purity Vishenwa almaarufu Pritty Vishy amesisitiza kwamba alimaliza masomo yake ya shule ya upili takriban miaka miwili iliyopita.

Katika chapisho kwenye ukurasa wake wa Instagram siku ya Ijumaa, mrembo huyo mwenye umri wa miaka 22 alisema kwamba alifanya mtihani wake wa KCSE mnamo Machi 2022.

Alibainisha kuwa watu wengi huwa na shaka kila anaposema kwamba alimaliza elimu ya sekondari miaka miwili tu iliyopita.

"Ninapenda jinsi watu hawaniamini ninaposema nilimaliza masomo yangu ya fomu 4 mnamo 2022 Machi," Pritty Vishy alisema chini ya video ya kumbukumbu ambayo alishiriki kwenye mtandao wa Instagram.

Katika video hiyo ambayo alikuwa amechapisha kwa mara ya kwanza mnamo Juni 2022, mpenzi huyo  wa zamani wa mwimbaji Stevo Simple Boy alisikika akizungumzia msisimko wake wa kumaliza shule.

“Kwa hiyo leo ninayo leo nina Kemia. Ijumaa ijayo nafanya Biology Practical kisha nimalize shule. Ni hisia bora zaidi. Kuamka sijui saa kumi unaenda shule, ni hisia mbaya zaidi. Ndiyo, Pritty Vishy ni mwanafunzi,” alisema kwenye video hiyo ya kumbukumbu.

Aliendelea kuzungumza kuhusu  jinsi alivyokuwa mkubwa zaidi katika darasa lao na jinsi mama yake angeweza kumtia moyo kutokata tamaa na masomo yake.

Kweli, ni kweli kwamba katika siku za nyuma watu wametilia shaka, si tu wakati Pritty Vishy alipomaliza shule bali umri wake pia.

Takriban miezi mitatu iliyopita, Pritty Vishy alifurahi kufikisha umri wa miaka 22. Siku yake ya kuzaliwa ilikuwa tarehe 3 Oktoba na kwa tukio hilo maalum, mama yake alipaswa kurudi kutoka Saudi Arabia ambako alikuwa akifanya kazi kama mfanyakazi wa nyumbani.

Mwanasosholaiti huyo mzaliwa wa Kibra alishukuru kwa miaka yake 22. Wiki nzima alikuwa akishiriki video kwenye TikTok yake, akitoa shukrani kwa miaka yake ya ujana.

"22 inaonekana nzuri kwangu tayari," akiongeza, "Mtoto ako 22yrs on Tuesday eiii❤️‍���"

Mashabiki hata hivyo hawakushawishika kuwa ana umri wa miaka 22 na walisema mengi katika sehemu ya maoni.

Akijibu maoni hayo ya kejeli, alionya watu kwenye video nyingine, "Mtu aniambie sikai 22yrs mtaniambia kaa ni nyinyi mlinizaa������"