logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Azziad azungumzia kukejeliwa mitandaoni baada ya umaarufu

Mwanamitindo Azziad Nasenya amezungumza jinsi alivyokejeliwa na kudhalilishwa mitandaoni pindi tu alipopata umaarufu mapema mwaka 2020.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri03 February 2022 - 08:24

Muhtasari


• Mwanamitindo Azziad Nasenya amezungumza jinsi alivyokejeliwa na kudhalilishwa mitandaoni pindi tu alipopata umaarufu mapema mwaka 2020.

• Nasenya alipata umaarufu baada ya mkanda wa video akicheza densi ya kibao ambacho msanii Femi One alimshirikisha Mejja, almaarufu Utawezana kusambazwa mitandaoni kwa wingi mno.

Mwanamitindo Azziad Nasenya amezungumza jinsi alivyokejeliwa na kudhalilishwa mitandaoni pindi tu alipopata umaarufu mapema mwaka 2020.

Nasenya alipata umaarufu baada ya mkanda wa video akicheza densi ya kibao ambacho msanii Femi One alimshirikisha Mejja, almaarufu Utawezana kusambaa mitandaoni kwa wingi mno.

Mwanamitindo huyo ambaye anajulikana pakubwa kwa kuunda video fupi akicheza densi na kisha kuzitundika katika mtandao wa TikTok anasema alidhalilishwa sana mitandaoni kwa miezi mitatu mpaka kidogo aathirike kwa unyongovu.

“Ilikuwa ngumu mwanzoni, kwa watu kunikejeli mitandaoni. Nilikaribia kuathirika kwa unyongovu lakini kwa bahati nzuri nilikuwa karibu na watu walionijali na kunipenda na walinisaidia sana kushinda majaribu hayo,” alisema Nasenya katika hafla moja alipokuwa akizinduliwa kama balozi wa kampuni ya Bic Februari 1.

Nyota huyo wa TikTok anasema kuwa kwa sasa ashajua tabia ya watu wa mitandaoni na hata hashughuliki nao vile.

“Mwisho wa siku najua pia kwamba Yesu alidhalilishwa na kukejeliwa na kwa maana hiyo mimi siwezi tegemea kwamba nitakuwa mkamilifu. Si kila mtu ambaye atapenda kile unachofanya na vilevile si kila mtu ambaye atachukia kile unachofanya,” alisema Nasenya.

Nasenya alizinduliwa kama balozi wa Bic Jumanne Februari 1


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved