logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Simjui! - Rose Muhando akana mahusiano na Abraham Mutai

Rose Muhando amekana kumjua wala kuwa na mahusiano na mwanablogu Abraham Mutai

image
na Radio Jambo

Habari15 February 2022 - 09:29

Muhtasari


• Mwimbaji mashuhuri wa injili Rose Muhando amejitokeza wazi na kukana mahusiano ya kingono na mwanablogu Abraham Mutai

• Amesema hata hana ufahamu mwanablogu huyo ni nani na kusema hamjui.

Mwimbaji mashuhuri wa injili Rose Muhando amejitokeza wazi na kukana mahusiano ya kingono na mwanablogu Abraham Mutai ambayo yalisambazwa mitandaoni mwezi uliopita na baadhi ya Wakenya.

Akizungumza katika kituo kimoja cha redio nchini, Muhando amepuuzilia mbali madai ya kufanya ngono ya usiku mmoja  na mwanablogu huyo kwenye klabu kimoja huko Thika kama ilivyosemekana. Amesema hata hana ufahamu mwanablogu huyo ni nani na kusema hamjui.

"Mimi sijali na sijutii sababu sina hatia na wala sijawai kutia unajisi katika ardhi ya Kenya. Ajipange upya sababu amefeli,” alisema Muhando

Mwezi jana, mwanamme mmoja alimtuhumu Abraham Mutai kwa kufanya ngono na Rose Muhando kwenye klabu huko Thika na kusema kwamba yeye ndiye aliwaelekeza wawili hao kwenye chumba cha kukodisha.

"Huwa sipendi kujibu tuhuma za kijinga kama hizo kwa sababu si za kweli n ani za kipumbavu. Mimi hata simjui Abraham Mutai na sijawahi kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na yeye. Aseme tu kama ananipenda hapo sawa,” alisema Muhando.

Mwimbaji huyo amesema kwamba hata kama watu walimuona katika sehemu hiyo akikodisha chumba cha malazi hakuna tatizo kwani kila mara yeye anapokuwa nchini hukodisha chumba kwa ajili ya kulala kwani hana nyumba yake nchini Kenya.

Mwezi jana madai hayo yaliposambazwa mitandaoni, mwanablogu Abraham Mutai aliyapuuzilia mbali pia na kusema kwamba wale waliokuwa wakiyasambaza ni wenye walikuwa wametofautiana kisiasa, haswa ikizingatiwa kwamba mwanablogu huyo anatofautiana vikali na sera za naibu rais William Ruto ambaye wanatoka eneo moja la mkoa wa bonde la ufa.

“Mimi nasisitiza vikali kwamba sikuwahi lala na Rose Muhando katika chumba namba 4 mjini Thika ama mji wowote… mawakili wangu watamtembelea huyo mpokezi katika hoteli hiyo ili kubaini ukweli,” alisema Mutai.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved