logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ponda raha mpenzi wangu wa zamani, maisha ni mafupi - Eudoxie amwambia Grand P

Eudoxie Yao amemtakia kila la Kheri Grand P baada ya kuona video akiogelea na mwanamke

image
na Radio Jambo

Habari21 February 2022 - 09:09

Muhtasari


• Eudoxie Yao amemtakia Grand P kila la kheri katika maisha baada ya video ya mwanamuziki huyo akiogelea na mwanamke mwingine

Mwanamitindo mwenye mwili mkubwa kutokea nchini Ivory Coast Eudoxie Yao amemtakia kila la kheri katika maisha aliyekuwa mpenzi wake Grand P, baada ya kumuona kwenye video akijivinjari katika kwenye bwawa la kuogelea na mwanamke mwingine.

Katika video hiyo, mwanamuziki huyo kutoka Guinea mwenye umbule dogo Zaidi la mwili amepakia video hiyo wakiogelea kwenye Facebook yake na kusema kwamba anajivinjari kadri ya uwezo wake kwani Maisha ni mafupi mno.

“Maisha ni kitu cha kuvutia sana, jibambe kadri ya uwezo wako. Mimi najivinjari kivyangu,” aliandika Grand P

Katika sehemu ya kutoa maoni, aliyekuwa mpenzi wangu ambaye pia ni mwanamitindo Eudoxie Yao ameandika ujumbe wa kumtakia kila la kheri anapojibamba katika Maisha.

“Jibambe mpenzi wangu wa zamani, Maisha ni mafupi,” aliandika Eudoxie Yao.

Fununu za kuachana kwa wawili hao zilizuka wakati wa mashindano ya AFCON nchini Cameroon mapema mwezi Februari wakati mwanaume huyo mdogo alionekana akiwa na wanawake wengi wakisherehekea ngarambe hiyo, jambo linalotajwa kumkera Yao na kumpelekea kufanya maamuzi ya kumuacha Grand P.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved