logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Erick Omondi amsifia Edgar Obare kwa 'kuwaanika' wasanii

Mcheshi Erick Omondi amemsifia Edgar Obare kwa kuwaanika wasanii.

image
na Radio Jambo

Makala23 March 2022 - 05:11

Muhtasari


• Erick Omondi alisema kwamba anaunga mkono michakato ya mwanablogu Edgar Obare kuendelea 'kuwaanika' wasanii.

• Aliongezea kwamba kwa kiasi fulani mashabiki wanapaswa kufahamu hali ya maisha ya wasanii hao.

Eric Omondi

Mcheshi Erick Omondi kwa mara ya kwanza amempongeza mwanablogu Edgar Obare kwa harakati zake za kufichua siri za wasanii wengi humu nchini.

Akizungumza katika mahojiano na Spm Buzz, Omondi alisema kwamba Obare anapaswa kulipwa na kupewa heshima kwa kuwa amelisaidia gemu la burudani.

Omondi alishikilia kwamba mwanablogu huyo amesaidia pakubwa katika kuchangamsha sanaa, na kumtaka aendelea na juhudi hizo.

"Edgar amekuwa mtu wa maana katika sanaa yetu, anapaswa kupewa heshima yake," Erick Omondi alisema.

Vilevile alisema kwamba mtu anapokuwa maarufu, basi kwa kiasi fulani mashabiki wanatakiwa kujua kinachoendelea katika maisha yake.

Aliwataka wasanii kutompiga vita Obare na badala yake kumpa sapoti ili sekta ya burudani izidi kufana.

Ifahamike kwamba Obare kwa muda mrefu sasa, amekuwa akiweka wazi kwa umma siri za wasanii jambo ambalo kwa mara kadhaa limempelekea kujikuta matatani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved