logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Erick Omodi amnunulia 'mpenzi' wake gari katika birthday yake

Erick Omondi amemnunulia 'mpenzi' wake gari katika siku yake ya kuzaliwa.

image
na Radio Jambo

Habari30 March 2022 - 05:59

Muhtasari


• Mcheshi Omondi amemnunulia 'mpenzi' wake gari katika siku yake ya kuzaliwa.

• Alisema ni zawadi ndogo ya kumpongeza kwa bidii yake.

Mcheshi Erick Omondi amewashangaza mashabiki baada ya kumnunulia 'mpenzi' wake gari katika siku yake ya kuzaliwa.

Kupitia ujumbe aliochapisha katika ukurasa wake wa Instagram, Omondi alisema kwamba gari hilo lilikuwa zawadi ndogo kwa Lynne kutokana na bidii yake katika mishe zake.

"Nimemnunulia Lynne zawadi ndogo ya siku yake ya kuzaliwa. Napenda bidii yake na najua ataenda mbali," Omondi alisema.

Mashabiki hawakuachwa nyuma huku wakijitokeza kwenye 'comment section'  kumpongeza Omondi kwa hatua hiyo na kumtakia Lynne heri katika siku yake ya kuzaliwa.

Aidha kuna wale walimtupia cheche wakisema kwamba penzi lao halitadumu kwa muda mrefu.

"Mtaachana tu," shabiki mmoja aliandika.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved