logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Zitakuwa madukani hivi karibuni" Stevo Simple Boy kuanza biashara ya sharubati

“Na Mungu akituzidia zitakuwa madukani hivi karibuni tukuwe freshi barida,” aliandika staa huyo aliyetamba na kutambulika na wengi kwa wimbo wake wa kwanza wa ‘Mihadarati’

image
na Radio Jambo

Habari12 July 2022 - 13:34

Muhtasari


• Msanii huyo kutoka Kibera amekuwa akipiga hatua ambapo awali alianzisha kuuza sweta zenye maneno 'Freshi Barida'.

Msanii kutika Kibera, Stevo imple Boy

Mwanamuziki wa kizazi kipya Stivo Simple Boy aanzidi kukwea kwenye ukwasi kupitia muziki. Hii ni baada ya kutangaza kwamba hivi karibuni atazindua kampuni yake ya kutengeneza sharubati na kuita kinywaji hicho kwa jina la ‘Freshi Barida’

Akiandika kupitia Instagram yake, Simple Boy alidokeza kwamba hivi karibuni Mungu akimjaalia kinywaji hicho kitakuwa madukani.

“Na Mungu akituzidia zitakuwa madukani hivi karibuni tukuwe freshi barida,” aliandika staa huyo aliyetamba na kutambulika na wengi kwa wimbo wake wa kwanza wa ‘Mihadarati’

Staa huyo kutokea mtaa wa mabanda wa Kibera jijini Nairobi alipozuka katika fani ya muziki mnamo mwaka 2019, wengi waligeuka umbile na muonekano wake kuwa kioja cha kuchekesha, wengine kumuona kama kinyago ila hakufa moyo na masimango hayo ya mitandaoni, bali alitia nta kwenye masikio na kuzidi kuchapa kazi kwa jitihada kubwa.

Aidha mwaka huu haujamwanzia vizuri baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Pritty Vishy katika njia ya kuchafuana mitandaoni kwa cheche za nguoni huku Simple Boy akimtaja kuwa alikuwa mchepuko mwenye zaidi ya wanawake 50.

Msanii huyo pia alisemekana kudhulumiwa na usimamizi wa awali wa kazi zake za muziki ambapo uvumi ulizuka pia kwamba hadi akaunti zake za mitandaoni zilizamishwa na usimamizi huo ambapo aliamua kuanza upya.

Licha ya changamoto zote hizo, Simple Boy bado alizidi kung’ara ambapo aliachia kibao chake kwa jina ‘Freshi Barida’ na kuteka anga nchini pakubwa, mafanikio yaliyompa motisha ya kuanza kuuza sweta zenye nembo hiyo ya ‘freshi barida’

Wiki jana pia alitoa ‘remix’ ya ngoma hiyo ambayo safari hii aliwashirikisha mastaa wa gengetone kama vile Mejja, Exray miongoni mwa wengine, ngoma ambapo chini ya siku nne imefanya vizuri mno kwenye mtandao wa YouTube.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved