logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nilipewa 500K, nikajengea wazazi wangu nyumba kijijini" - Stevo Simple Boy

“Zilikuwa nusu milioni, kutoka kwa lile tangazo la OdiBet, nilipewa na kikajengea wazazi nyumba kijijini,” Stevo Simple Boy.

image
na Radio Jambo

Habari23 July 2022 - 09:56

Muhtasari


• Simple Boy alisema usanii unalipa kama msanii ni mnyenyekevu na hana vituko vya kumharibia jina.

Msanii Stevo Simple Boy akiwa katika mahojiano na Mwafreeka

Msanii wa moto kabisa sasa hivi nchini Kenya, Stevo Simple Boy amefichua kwamba wasimamizi wake wa awali katika kazi zake za muziki, Made In Kibera walimpa pesa nyingi sana baada ya maelewano ya kufanya tangazo la kampuni moja ya ubashiri humu nchini.

Akizungumza kwenye podcast ya aliyekuwa mtangazaji Mwafreeka, Simple Boy alisema kwamab Made In Kibera walimpa kiasi cha nusu milioni pesa taslimu za benki kuu ya Kenya na akafurahia sana ambapo alitumia kitika hicho kuwajengea wazazi nyumba.

“Kwa hiyo pesa nyingi kabisa ulipatiwa ukiwa huko, yaani umetumbuiza halafu ukapatia kwamab chukua hii, zilikuwa kiasi kipi?” Mwafreeka alimuuliza msanii huyo.

“Zilikuwa nusu milioni, kutoka kwa lile tangazo la OdiBet, nilipewa na kikajengea wazazi nyumba kijijini,” Stevo Simple Boy.

Aidha msanii huyo alipuuzilia mbali kauli kwamba usanii haulipi na kusema kwamba katika usanii kuna pesa iwapo msanii ako mnyenyekevu na hana vituko vingi vinavyomwandama na kulitia jina lake mchangani.

Msanii huyo anazidi kukwea ngazi za mafanikio tangu miezi michache walipotengana na aliyekuwa mpenzi wake, Pritty Vishy ambapo walimwaga mtama wa siri zao mitandaoni, kila mmoja akijaribu kulisafisha jina lake kwa kumkandia mwingine chini.

Hivi majuzi, Stevo Simple Boy alitangaza mipangi ya maisha yake na kusema kwamba hivi karibuni atafungua kampuni ya kutengeneza sharubati kwa jina Freshi Barida, jina ambalo amelitoa kwa wimbo wake uliomfanya kujulikana zaidi mwaka huu mpaka kubidi kufanya ‘remix’ ya ngoma hiyo akiwashirikisha wasanii wengine kutoka humu nchini.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved