logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nataka uzae mapacha wa kike" Mtoto wa Yvette Obura amwambia Diana Marua

Diana Marua alipakia video akiwauliza watoto wake kuhusu mtoto ambaye wanatarajia kuzaliwa, wiki mbili baada ya kuweka wazi kwamba anatarajia mtoto mwingine.

image
na Radio Jambo

Habari26 July 2022 - 11:01

Muhtasari


• Mueni Bahati alisema anatarajia watoto mapacha ambao wote watakuwa wa kike.

• Diana Marua alisema yeye hana shinda na mtoto yeyote ambaye Mungu atambariki naye.

Mwanamuziki Diana Marua na familia yake

Mwanamuziki wa kufoka na mkuza maudhui Diana Marua amepakia video kwenye YouTube yake akiwauliza watoto wake wanne kuhusu maoni yao ya yule mtoto ambaye wanatarajia, wiki mbili baada ya kuutangazia ulimwengu kwamba anatarajia mtoto mwingine.

Watoto hao wanaonekana kufurahia huku wakisema kwamba tangu aweke wazi kwamba ni mjamzito, watoto wake wamekuwa wakirudi kutoka shuleni kila jioni na kutarajia kupata mtoto huyo ameshazaliwa.

Morgan, ambaye ni mtoto Bahati alimpaka kutoka mitaani alikuwa wa kwanza kuulizwa iwapo angependa kijacho awe mtoto wa kike au wa kiume, ambapo kijana huyo mtanashati alisema bila kubabaika kwamba anatarajia mtoto atakayezaliwa awe ni anataka mtoto awe ndugu yake wa kiume.

“Mimi nataka awe wa kiume kwa sababu napenda tu wavulana,” alisema Morgan.

Alisema kwamba bado anampenda ndugu yake mdogo Majesty lakini pia anataka ndugu mwingine wa kiume.

Aliyeshangaza ni mueni ambaye ni mtoto ambaye Bahati alizaa na mwanamke mwingine kwa jina Yvette Obura ambaye alisema kwamba yeye hatarajii kitu chochote chini ya mapacha na kusema kwamba anatarajia wote wawe mapacha wa kike mpaka akaomba Mungu awape mapacha hao.

Mtoto wake wa kwanza kwa kumzaa, Heaven Bahati alisema kwa upande wake angependa kumuona ndugu wa kike kwani wa kiume wanachosha tu.

“Mimi nataka mtoto ambaye ataitwa Heaven kama mimi ndio niwe nikimbeba na pia kulala na yeye,” alisema mtoto huyo.

Watoto hao hatimaye walimuuliza kama anataka mtoto wa kike au wa kiume na Diana Marua aliwajibu kwamba yeye hana tatizo na mtoto yeyote ambaye Mungu atampa kwani atashukuru tu pakubwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved