logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Yule dada nilikuwa naona kwa TV sasa naamka naye kitanda kimoja, ahsante Mungu" - Harmonize

“Hata yule dada (Kajala) tuliyekuwa tunamlipia shilingi 100 bandani na masala ili kumuona siku ikija runinga kijijini kwetu, sasa ninaamka na yeye na ananiita Daddy" - Harmonize.

image
na Radio Jambo

Habari27 August 2022 - 11:56

Muhtasari


• "Kutoka maisha ya kuenda mtoni kuteka maji kwa dumu kwa mguu na kubeba kichwani na ukifika unafua nguo unasubiri zikauke ili uzivae tena, ila sasa nashukuru nipo katika upeo wa muziki,” - Harmonize.

mSANII hARMONIZE AMSHUKURU Mungu kwa kumletea Kajala Masanja maishani mwake

Staa mmiliki wa lebo ya Konde Music Worldwide, Harmonize ni mtu mwenye kumbukumbu nyingi sana za enzi zake za utoto huku akimshukuru Mungu pia kuhusu vile vyote ambavyo amevipata katika maisha mpaka sasa.

Ijumaa kupitia instastories zake, Harmonize aliachia ujumbe mmoja mrefu na wa kugusa sana huku akisimulia jinsi alivyokuwa akienda mtoni kuteka maji kwa dumu na kubeba kichwani.

“Eeh Mungu, najua ninauliza vingi sana kila siku, ila tafadhai endeleeni kunibariki kwa kile ambacho nakihitaji. Kutoka maisha ya kuenda mtoni kuteka maji kwa dumu kwa mguu na kubeba kichwani na ukifika unafua nguo unasubiri zikauke ili uzivae tena, ila sasa nashukuru nipo katika upeo wa muziki,” Harmonize aliachia ujumbe wenye kumbukumbu za kuliza.

Pia akigusia huba lake na muigizaji mkongwe Kajala Masanja kwa kusema kwamba kitambo alikuwa anaenda kwenye banda kulipia filamu ili kumuona ila kwa sasa hivi wanaamka na yeye ndani ya kitanda kimoja, blanketi mmoja.

“Hata yule dada (Kajala) tuliyekuwa tunamlipia shilingi 100 bandani na masala ili kumuona siku ikija runinga kijijini kwetu, sasa ninaamka na yeye na ananiita Daddy, Mungu dua langu leo linaenda kwa wasio nacho kabisa,” Harmonize aliandika.

Harmonize na Kajala wanatarajia kufunga pingu za maisha hivi karibuni baada ya miezi michache iliyopita kuvishana pete za uchumba.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved