logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Willy Paul atangaza kupata mchumba, Jovial, aonya wapenzi wa kitambo

Paul alidaiawa kuwa na mazoea ya kumtumia ujumbe mwanadada ambaye ni mpenzi wa wenyewe.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 September 2022 - 04:30

Muhtasari


• Mwanamuziki huyo alisema kuwa hajali wanachoongea watu kwani yeye na mpenzi wake Jovial wanapendana kwa dhati.

 

Mwanamuziki Wilson Abubakar Radido almaarufu Willy Paul ayaongelea mahusiano yake na mwanamuziki anayedaiwa kuwa mpenzi wake wa sasa Juliet Miriam Ayub almaarufu Jovial.

Willy Paul alisema yeye na Jovial wamekuwa familia tayari na kuwa uhusiano wao hauwezi ukavunjwa.

Mwanamuziki huyo alisema kuwa hajali wanachoongea watu kwani yeye na mpenzi wake Jovial wanapendana kwa dhati.

"Hakuna kitu ambacho kitabadilika hata mkiongea,tushapendana na ni hivyo. Hii picha ya kifamilia iko aje?"alisema.

Aliwaonya na kuwakanya wanadada aliokuwa akiongea nao hapo awali kabla aanze uhusiano wake na Jovial akiwambia kuwa hayo ni mambo yaliyotendeka kabla ya kumpata Jovial.

Willy Paul aliwaambia wapambe kuwa hakuna kitu wataweza kufanya ili kumtenganisha na Jovial ikiwemo kufunga na kwenda kwenye maombi.

"Na kwa wale wasichana pengine tulikuwa na mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea, poleni sana nishapenda kwengine,"alisema.

Msanii huyo aliongeza kuwa Kenya ndio mahali pekee ambapo mtu akipenda ama kuwa kwenye mahusiano linakuwa jambo kubwa .

Haya yaliweza kutendeka baada ya Willy Paul kusemekana kuwa na mazoea ya kumtumia ujumbe mwanadada ambaye ni mpenzi wa wenyewe.

Willy Paul aliwafokea watu baada ya suala hilo kuenea mtandaoni na kusema kuwa yeye na Jovial ni kitu kimoja na hawawezi wakatenganishwa na jambo lolote lile.

"Haha kwani mimi kuwa kwenye uhusiano imeumaje watu. Endeleeni, mimi nishapata wangu," alisema.

Jovial pia aliweka wazi picha yake na Willy Paul mtandaoni na kusema kuwa bado wataendelea kuwa kwenye mahusiano hata watu waseme nini.

"Bado tupo sana, kiwiliwili changu,"alisema.

Hata baada ya mahaba haya yote wawili hawa wameonyesha mitandaoni mashabiki wao wengine bado wanashuku mahusiano hayo na kusema kuwa ni kiki ya wimbo mpya ambao Willy Paul na Jovial wanatafuta.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved