logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nyota ya Mandonga yazidi kung'aa, azawadiwa gari baada ya pambano Nairobi

Mandonga alimshukuru mfanyibiashara huyo kwa zawadi hiyo na kusema ni ndoto.

image
na Radio Jambo

Habari18 January 2023 - 06:46

Muhtasari


• Mwanabondia huyo alikanusha madai kuwa alikuwa hajalipwa na kusema kuwa pamoja na kamati yake, walikuwa wamelipwa kikamilifu.

Mandonga apata gari

Bondia kutoka Tanzania Karim Mandonga amesemekana kuzawadiwa gari na mfanyibiashara maarufu nchini humu, siku chache tu baada ya kung’ara katika pambano la ngumi jijini Nairobi.

Mandonga alikuwa anapambana na Mkenya Daniel Wanyonyi ambaye alimshinda katika raundi ya 5 kwa muondoano wa kitaalamu.

Bondia huyo mwenye kubwabwaja sana alitangaza promo ya pambano hilo tangu wiki kadhaa zilizopita huku akisema kuwa ngumi aliyokuwa amemuandalia Wanyonyi ilikuwa na asili kutoka kwa milipuko ya mabomu katika vita vya Urusi na Ukraine kwa jina Sugunyo.

Na kweli kwa maneno yake, aliweza kumchachawiza Wanyonyi na kuzidisha tantarira zake baada ya kushinda.

Mengi mazuri yamemfuata na baada ya kudaiwa kuzawadiwa gari, Mandonga kupitia Instagram yake alimshukuru mfanyibiashara huyo huku akisema kuwa kwa muda mrefu ilikuwa ni ndoto yake kupata usafiri wake binafsi, ndoto ambayo imefanikishwa baada ya pambano la Kenya – ambalo lilikuwa la ushindi wake wa kwanza nje ya nchi.

“@dicksoundmall BOSI hii kwangu ni kubwa sana nilikuwa na mawazo ya kumiliki usafiri wangu lakini Leo umeweza kunikamilishia Moja Kati ya ndoto zangu @dicksoundmall anae toa kila siku mungu nae humpa kila siku shukran kubwa sana kaka ALLAH akuzidishie zaidi boss wangu,” Mandonga alisema.

Awali kulikuwepo na taarifa kuwa mwanabondia huyo hakuwa amelipwa bali alikuwa anafanya kwa kujinoa tu lakini madai hayo yalifutiliwa mbali na promota wake ambaye alisema fedha zote alizipokea yeye na kumtaka mchekeshaji Eric Omondi kuomba radhi ndani ya siku saba kwa kudanganya kuwa Mandonga hakulipwa.

“Mimki ndio niliipokea pesa yote ninayo, na huo ni uongo. Eric Omondi tunaweza kumchukulia hatua kwa sababu anatuchafulia jina,” Promota alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved