logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Drake atangaza kurekodi kwa studio yake ni shilingi milioni 33 kwa saa moja

Tayari rapa mmoja kwa jina Riff Raff ameshaweka ombi la masaa mawili kwa $500000.

image
na Radio Jambo

Habari03 April 2023 - 06:34

Muhtasari


• Studio hiyo iko nyumbani kwake huko Kanada Toronto na ina vifaa vyote anavyotumia Drake.

Drake atangaza bei ya kurekodi kwenye studio yake.

Msanii maarufu kutoka Canada, Drake anawapa mashabiki wa muziki na wasanii wanaotarajia kuingia studioni kurekodi, fursa ya kipekee.

Katika hali ya kushangaza, Drake ameorodhesha studio yake ya nyumbani kwenye Stufinder kwa $250,000 USD kwa saa, kiasi sawa na shilingi milioni 33 za Kenya kwa saa.

Studio hiyo iko nyumbani kwake huko Kanada Toronto na ina vifaa vyote anavyotumia Drake. Katika Tweet hapo awali, Stufinder walisema kwamba "tunafahamu studio ya nyumbani ya Drake iliyoorodheshwa kwenye App yetu. Kwa sasa tunathibitisha kwamba Drake au timu yake walishiriki katika orodha hiyo."

Baadaye, program hiyo ilionekana kuthibitisha katika Tweet nyingine iliyoripoti tangazo la Toronto na kwamba watumiaji wake "kamwe hawahitaji kuwa na wasiwasi kuhusu kulaghaiwa kwa Stufinder."

Maelezo ya tangazo hilo yanasomeka, "Studio ya kibinafsi ya Drake ya kurekodi nyumbani. Studio ya nyumbani inajumuisha vifaa maalum. Hakuna mhandisi aliyejumuishwa. Kipengele cha Drake hakijajumuishwa.”

Wakati orodha hiyo ikithibitisha kuwa Drake wala mhandisi wa sauti atajumuishwa kwenye booking hiyo, inaonekana tayari kuna watu wanaopenda nafasi hiyo, huku rapper Riff Raff akiwa wa kwanza kuweka ombi la masaa mawili kwenye studio ya nyumbani kwa Drake kwa $500,000 USD.

Inabakia kuonekana ni muda gani uorodheshaji utakuwa mtandaoni na ni nani mwingine atakayeweka ombi la kutaka kurekodi wimbo kwenye studio hiyo inayotajwa kuwa ya kifahari.

Tangazo la Drake linakuja siku moja tu baada ya bendi maarufu kutoka Kenya – Sauti Sol – kutangaza kwamba wamefanikiwa kuwahi collabo na msanii huyo kutoka Kanada, ila hawakufunguka maelezo Zaidi iwapo walirekodi ngoma kwenye studio yake au walimtafutia studio nyingine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved