Nicah the Queen anadaiwa kuvujisha ujumbe wa faragha uliotumwa kwa mchumba wake Dj Slahver. Maandishi hayo yanaonyesha mwanamke akitaniana na kumuuliza Slahver kama anaweza kumnunulia kahawa.
"Halo, Dj. Naona wewe ni ballin tu. Naweza kukununulia kahawa?" anamuuliza, lakini Slahver alimuuliza nia yake, "Kwa nini?"
Alimwambia huku mwanamke huyo akimjibu, "Lazima kuwe na kwa nini? Ninakupenda," mwanamke wa ajabu alimwambia Slahver.
Hili lilimkasirisha Nicah ambaye aliposti picha ya skrini ya mazungumzo hayo. Nicah alidai kuwa alihitaji kufichua mwanamke huyo kwa kumtumia ujumbe mchumba wake ili kuwaonya wengine ambao wanaweza kujaribu.
"Maisha ni ya kuchekesha sana!! Kikulacho ki nguoni mwako!! Huyu ni rafiki yangu mkubwa sana….. Mtu Mashuhuri anayejaribu kutaniana bila mimi kujua kwenye Slahver!! Umekuwa ukisisitiza nimlete Slahver kwa chajio kwako kumbe unataka kumchukuwaπ"
Lakini mashabiki hawaamini kuwa hii ni DM halisi. Wanasisitiza kuwa Nicah anatafuta ufuasi sana na ni ujumbe wa uongo.
Nicah aliongezea, "Ukaona I'm not interested ukaslide kwa DMππππ Ati I see y'all are ballin??? Ulitaka tuteseke ama?? πππππ weeeh najionea mengi!! Ati bestie bestie ππππmkakae na huko mimi sitaki marafiki madem tena!!Sitaki πππ @slahverdon wasikuchukuwe hawa watu!!"
Maoni haya yalimkashifu Nicah:
keen_eliza061 Tunajua unajicht tu uyo jamaa wako SI mhandsome ataπpungunguza mdomo....
ellaria2011 Niccah always chasing clout. Who believes this? Huyo Ni wewe umetext .
hilda_kalya I'm sure hii ni pseudo account ya uyo Jesus girl tu kwa sababu sidhani kuna mtu anaeza taka uyo dj smtππππ
hilda_kalya @sha.mi.ne hakuna mtu anaeza taka dj actually ππππ
kerrykerry58 Hakiii wewe unajiita jesus gal but u such a pathological liar utakuja kupigwa na radi… sasa hicho kimwanaume chako sooo broke unakaa wewe ndio bread winner who can throw shorts on him??? Yaan unajiona kama uko na superstar vile nkt.