logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanasha Donna afunguka ukweli kuhusu kuhisiwa kupata mpenzi mpya Mnigeria

Tanasha amekuwa akificha hali yake ya kimapenzi tangu kuachana na Diamond miaka 3 iliyopita.

image
na Radio Jambo

Habari22 May 2023 - 05:16

Muhtasari


• Tanasha ana mtoto mmoja na Diamond Platnumz lakini baada ya kuachana naye takribani miaka 3 iliyopita, hajawahi muonesha mpenzi mpya.

Tanasha akanusha kuwa na mpenzi mpya

Mtangazaji na mwanamuziki Tanasha Donna ameibua gumzo tena kuhusu picha aliyoipakia ya mwanamume mmoja anayedhaniwa kuwa raia wa Nigeria wiki saba zilizopita.

Tanasha alilazimika kunyoosha maelezo baada ya blogu moja ya humu nchini kuchokonoa picha hiyo na kudai kwamba wengi wa wafuasi wa Tanasha wamekuwa wakihisi ndiye mpenzi wake mpya.

Katika picha hiyo, Tanasha alikuwa amemwagia makopakopa mwanamume huyo huku akisema kuwa asingeweza kuwa na subira Zaidi kama hajamuona, maneno ambayo jamaa huyo alimjibu kwa mahaba huku akimtaja waziwazi kama mpenzi wake.

“Jiangalie, nina fahari sana kwako, hivi karibuni nitakuja Mungu akiridhia,” Tanasha aliandika.

“Mpenzi wangu Tanasha Donna nashukuru, nina hamu sana ya kupatana nawe tena,” Jamaa huyo kwa jina Zpxnso kwenye Instagram aliandika.

Hata hivyo baada ya watu kuhisi wanatoka kimapenzi, mama huyo wa mtoto mmoja alijitokeza wazi na kukana akisema kuwa ni rafiki tu na watu wasiwe wanakweza vitu vidogo kuwa vikubwa.

“Hapanaa, acha hizo sisi ni marafiki,” Tanasha alisema.

Wiki mbili zilizopita, msanii huyo ambaye ni mzazi mwenza wa Diamond Platnumz kutoka Tanzania aligonga vichwa vya habari alipodokeza kuwa hana furaha kuishi nchini Kenya na kuwa alikuwa na mpango wa kuhama kabisa pamoja na mwanawe kwenda nchi za mbali.

Tanasha alisema kuwa habari mbaya kila uchao nchini zilimfanya kujihisi hayuko katika mazingira salama kabisa kwake na mwanawe.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved