logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Christiano Ronaldo akiri kuwa mara kwa mara huwa anajitafuta kwenye google

Ronaldo kwa sasa yuko na umri wa miaka 38.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri06 September 2023 - 11:18

Muhtasari


• “Ndio nimewahi jitafuta mara nyingi tu,” Ronaldo alijibu na kifaa hicho cha kugundua uongo na ukweli kikakubaliana na jibu lake.

 
• Mchezaji huyo pia alikiri kwamba yeye mara nyingi hula vyakula vya mtaani.

Ronaldo

Siku moja iliyopita, mchezaji namba moja duniani kwa muda wote Christiano Ronaldo alikuwa gumzo la mitandaoni baada ya shirika la biashara za fedha Binance kufichua mahojiano waliyofanya na mchezaji huyo nguli kutoka Ureno.

Ronaldo kwa muda sasa amekuwa balozi wa mauzo wa kampuni hiyo na safari hii waliamua kumweka kwenye kiti moto wamtaka kujibu maswali yao moja kwa moja kwa kutumia ndio au hapana bila kujieleza kisha wanaweka jibu lake kwenye mtandao wa kugundua uongo na ukweli.

Katika moja ya maswali, mhoji Andy alimuuliza iwapo amewahi jitafuta kwenye mtandao mkuu wa kutafuta vitu mbali mbali wa Google.

“Ndio nimewahi jitafuta mara nyingi tu,” Ronaldo alijibu na kifaa hicho cha kugundua uongo na ukweli kikakubaliana na jibu lake.

Mchezaji huyo pia alikiri kwamba yeye mara nyingi hula vyakula vya mtaani.

Ronaldo alikiri pia kwamba ligi kuu ya premia nchini Uingereza ni moja ya ligi ngumu Zaidi duniani, jibu ambalo lilikuwa kweli kulingana na kifaa cha kugundua uongo na ukweli.

Nahodha huyo wa Ureno ambaye kwa sasa ni wa moto kuiwajibikia timu ya Al Nassr ya Saudi Arabia alisema kwa kusisitiza kwamba analenga kucheza soka hadi pale atakapofikisha umri wa miaka 40.

Ronaldo kwa sasa yuko na umri wa miaka 38.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved