Aslay: kuachana na mpenzi wangu Tessy kuliniacha na machungu mno

Licha ya kutengana na Tessy, Aslay amesema wanashirikiana katika malezi ya mtoto wao

Muhtasari

•Aslay amesimulia machungu yaliyomkuta baada ya kuachana na mke wake Tessy ambaye walibarikiwa pamoja mtoto mmoja.

ASLAY/INSTAGRAM
ASLAY/INSTAGRAM

Msanii wa nyimbo za Bongo Tanzania  Aslay jina lake kamili Aslay Isihaka Nassoro, amesimulia machungu yaliyomkuta baada ya kuachana na mke wake Tessy ambaye walibarikiwa pamoja mtoto mmoja.

Aslay alihojiwa na kituo kimoja cha runinga cha Tanzania ambapo alisimulia maisha ya mapenzi akiwa na umri mdogo wakati jina lake lilijulikana kwa nyimbo zake zilizovuma .

"Nilipokosana na mama wa mtoto wangu kwa kweli maisha yangu yalirudi nyuma kwa muda nilishikwa na msogo wa mawazo jambo ambalo lilinifanya kutotokea kwa umma kwa wakati nilikataa hata mahojiano ya moja kwa moja".Aslay alisema.

Mwimbaji huyo mashuri wa bongo alisema kilichomfanya kukumbwa na mawazo tele ni mtoto wake mdogo aliyezoea kucheza naye na wakati ndoa yake ilivunjika alizidi kukumbuka furaha na upendo wa mwanaye.

"Kwa kweli iliniuma kwa kuwa nilikuwa na malengo na mpenzi wangu ndoto yetu ilikuwa kubwa kufanikishwa maisha ya ndoa pamoja ,mke wangu alipoodoka kila siku nilidhani atarejea tena niliwatuma watu wa familia akiwemo babangu waongee naye lakini jambo ili halikufua dafu",msanii huyu aliwaambia wanahabari .

Wakati mwanahabari wa Ayo Tv alipotaka kujua mahusiano yao kwa sasa, mwimbaji huyu wa Bongo alidokeza kwamba kwa sasa mahusiano yao ni kulea mtoto tu, jambo ambalo alisema yeye pamoja na aliyekuwa mpenzi wake Tessy wanashirikiana licha ya kutengana.