logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Bado niko single" Mulamwah akanusha kufunga harusi na rafiki yake Ruth K

“Kule kwa kina Bestie nilienda tu kutembea kwa vile pia yeye anajua kwetu lakini wali overreact,"

image
na Davis Ojiambo

Burudani03 November 2023 - 07:52

Muhtasari


  • • Mchekeshaji huyo pia aliwapiga mashabiki wake usinga wa uongo machoni akikataa kuzungumzia uvumi kwamba Ruth K ana mimba.
Mulamwah na mpenziwe

Mchekeshaji Mulawah amekanusha dai la kufunga harusi na rafiki wake wa karibu Ruth K wikendi iliyopita.

Katika mahojiano na waandishi wa habari za mitandanoni, Mulamwah alikanusha kwamba shughuli iliyuomuonesha wikendi akiwa na bestie wake Ruth K katika kile kilichoonekana kama harusi ya kitamaduni wala si harusi.

Alisisisitiza kwamba yeye bado yuko single na hana mpenzi akisema kwamba mambo ya Ruth K na mpenzi wake yeye hawezi ingilia.

“Kule kwa kina Bestie nilienda tu kutembea kwa vile pia yeye anajua kwetu lakini wali overreact, kufika nikapata maturubai ikabidi tu imekuwa sherehe lakini mimi sikutarajia,” alisema.

Mchekeshaji huyo pia aliwapiga mashabiki wake usinga wa uongo machoni akikataa kuzungumzia uvumi kwamba Ruth K ana mimba.

“Mimi sijui kama ako na mimba, hayo ni mambo yake na mpenzi wake, siwezi ingilia maisha yake, ni mwenyewe kuamua kufichua mimi siwezi zungumzia. Mimi kusettle ni mipango ya Mungu, kwa sasa hivi ni kutafuta pesa. Mimi nakuwa single muda wote, sina mpenzi,” alisema.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved