Vera Sidika ndio changuo langu Kenya Harmonize asema

Harmonize asimulia hisia zake kwa mwanasosholaiti Vera Sidika

Muhtasari

•Msanii huyo kwa kauli yake alimsifu Vera Sidika akisema iwapo angepata nafasi ndiye mwanadada wa Kenya ambaye siku zote angemchangua kama mpenziwe. 

Vera Sidika na Harmonize
Vera Sidika na Harmonize
Image: Facebook

Staa wa Bongo, Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize amefunguka kwa kusema kuwa mwanasosholaiti Vera Sidika ndio mwadada  nchini Kenya anyeweza kumchumbia iwapo angeaza kuchumbiana nchini.

Msaanii huyo maarufu nchini Tanzania alisema  hayo wakati alipokuwa akitumbuiza wafuasi wake wa Kenya katika eneo moja la burudani mjini Thika.

Harmonize alifunguka hisia zake kwa Vera  Sidika wakati alipokuwa akiwasifu wanadada wa Kenya waliokuwa wakinengua viuno huku wakimshabikia alipokuwa akitumbuiza jukwaani.

"Mara kwa mara mimi hujiuliza kwanini sijawahi chumbia warembo wazuri wa Kenya,kumbe nakosa mengii aaaaah...kuna manzi mmoja wa Nairobi nammezea sana siku nitalewa nitasema ni nani ....kuna mtu ameniambia Vera Sidika hana mchumba ni kweli,"aliuliza.

Msanii huyo kwa kauli yake alimsifu Vera Sidika akisema iwapo angepata nafasi ndiye mwanadada wa Kenya ambaye siku zote angemchangua kama mpenzi wake.

Harmonize alikuwa nchini Kenya kwa ziara ya siku mbili kwa tamasha moja ambalo aliwatumbuiza wafuasi wake,huku akisema kuwa mji wa Nairobi ndio moja kati ya miji mikuu amepata nafasi ya kutumbuiza mara nyingi.