logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mrembo mtangazaji afungua paybill kuchangiwa pesa za mazishi ya paka wake wa kiume

Alifungua paybill na kuwaomba watu kuchangisha pesa zisizozidi 20 bob.

image
na Davis Ojiambo

Burudani20 January 2024 - 08:13

Muhtasari


  • • Mashabiki wake katika mtandao huo walijibu instastory hiyo wakimtaka kuweka namba ya kutuma michango kwa ajili ya mazishi ya paka Mimi.
Natalia Githinii afiwa na paka

Mrembo Natalia Githinji ambaye ni mtangazaji katika kituo kimoja cha redio za mjini humu nchini anaomboleza kifo cha paka wake wa kiume kwa jina Mimi.

Githinji kupitia uurasa wake wa Instagram Story, alichapisha bango la kuomboleza kifo cha ghafla ya mnyama huyo pendwa akisema kwamba alikuwa amesalia na mwezi mmoja tu kumaliza miaka miwili tangu alipokutana naye kwa mara ya kwanza.

“Kwa ajili ya kumbukumbu ya upendo ya Mimi, Nilimkuta mara ya kwanza Februari mosi 2022 lakini amefariki Januari 17 mwaka 2024, mtoto wetu mpendwa,” Githinji alindika kwenye bango hilo.

Mashabiki wake katika mtandao huo walijibu instastory hiyo wakimtaka kuweka namba ya kutuma michango kwa ajili ya mazishi ya paka Mimi.

Githinji aliwajibu akisema kwamba hakuwa anataka pesa nyingi bali alitaka tu shilingi 20 kutoka kwa kila mmoja mwenye kuguswa ili kuandaa mazishi ya kufaa kwa paka wake mpendwa.

“Hata sitaki pesa nyingi, nataka shilingi 20 tu kutoka kwa kila mtu ili nipange mazishi… nitashukuru sana, nyinyi wote ni watu wangwana sana,” Githinji aliandika.

Wengine wakidhani ni mchezo, Bi Githinji alienda mbele na kuchapisha paybill kwa ajili ya miamala hiyo akisema kwamba angependa kumheshimu paka wake hadi pale anapoelekea mchangani.

“Mnaweza tuma meseji kwa DM yangu lakini msitume kitu chochote Zaidi ya shilingi 20. RIP mpenzi wangu Mimi, hii ni ya wale ambao waliitisha Paybill,” aliandika huku akifichua Paybill hiyo ambayo sisi hatuna idhini na mamlaka ya kuichapisha hapa.

"R.I.P Mimi, nakupenda vibaya sana mahn. Alikuwa daima kwa ajili yangu hasa baada ya upasuaji wangu na wakati endometriosis ilikua inaniweza .... wanyama ni uaminifu bora, wanastahili kila kitu. Naomba Mimi aende mbinguni 😇 😇" aliongeza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved