Mungai Eve adokeza kupata mpenzi mwingine, miezi michache baada ya kuachana na Trevor

Director Trevor alitangaza kuwa hayuko tena kwenye mapenzi na Eve mnamo Februari, akichukua umiliki wa pekee wa akaunti za mitandao ya kijamii walizoshiriki hapo awali.

Muhtasari

• Mungai amehama na kufungua akaunti mpya ambazo zilivutia wafuasi wengi ndani ya muda mfupi.

• Mwishoni mwa mwezi uliopita, akiwa Dubai, kijana huyo mwenye umri wa miaka 23 alizungumza kuhusu kuachana kwake na Trevor akisema hana hisia kali kwake.

MUNGAI EVE.
MUNGAI EVE.
Image: Instagram

Mkuza maudhui kwenye mtandao wa YouTube, Mungai Eve amedokeza kuwa hayuko single.

Mrembo huyo ambaye ni mpenzi wa zamani wa Director Trevor alifichua haya wakati alikuwa akiwajibu baadhi ya mashabiki wake kwenye chapisho lake la hivi majuzi.

Mmmoja alimuuliza kama ako na mpenzi au yuko single, swali ambalo alidakia kwa haraka akiweka wazi kwamba hayuko single.

"Babygal, wewe uko single?" mtumiaji huyo wa Instagram aliuliza na Eve akasema, "Mimi siko single."

Mungai eve
Mungai eve

Director Trevor alitangaza kuwa hayuko tena kwenye mapenzi na Eve mnamo Februari, akichukua umiliki wa pekee wa akaunti za mitandao ya kijamii walizoshiriki hapo awali.

Wapenzi hao wa zamani hata hivyo wamekataa kuangazia kilichosababisha kutengana kwao, ikizingatiwa kuwa walitimiza malengo ya wanandoa, na kuvutia pongezi na ukosoaji kila wakati.

Mungai amehama na kufungua akaunti mpya ambazo zilivutia wafuasi wengi ndani ya muda mfupi.

Mwishoni mwa mwezi uliopita, akiwa Dubai, kijana huyo mwenye umri wa miaka 23 alizungumza kuhusu kuachana kwake na Trevor akisema hana hisia kali kwake.

 

"Kila kitu kinatokea kwa sababu. Namshukuru Mungu kila siku mimi ni mtu wa kushukuru sana. Nilipo sasa hivi nashukuru sana, bila kusema kwamba pale nilipokuwa sikushukuru kusema tu mambo fulani hutokea maishani kwa bora. Nisingependa kukazia sana hilo kwa sababu ni ya zamani lakini naweza kusema mimi ni msichana mwenye furaha,” Eve alisema.

Alipoulizwa iwapo alikuwa anachumbiana na Eve alisema, "Kwa sasa, niko mahali pazuri zaidi, wakati mwafaka utakapofika na ninahisi kuwa naweza kushiriki sehemu yangu hiyo na familia ya mtandaoni nitakayoishiriki."