logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Naripoti moja kwa moja kutoka Garden City! "Khaligraph aifanyia mzaha nyumba yake kufuatia ukosoaji mitandaoni

“Habari ya asubuhi Kenya, ninaripoti moja kwa moja kutoka Garden City. Niko tayari kwa ushauri wenu," alisema.

image
na Samuel Mainajournalist

Mastaa wako12 November 2024 - 11:36

Muhtasari


  • Mwimbaji huyo wa kibao ‘Yes Bana’ alionyesha picha yake akiwa amekaa kwenye kochi kubwa kwenye sebule ya jumba lake kubwa la kifahari.
  • Khaligraph alitangaza kwa kejeli kwamba alikuwa katika maduka ya Garden City na kubainisha kwamba alikuwa tayari kusikiliza ushauri.


Rapa mahiri wa Kenya Brian Omollo almaarufu Khaligraph Jones ameungana na wanamtandao wengine kuifanyia mzaha nyumba yake kutokana na ukubwa wake.

Siku ya Jumanne asubuhi, mwimbaji huyo wa kibao ‘Yes Bana’ alionyesha picha yake akiwa amekaa kwenye kochi kubwa kwenye sebule ya jumba lake kubwa la kifahari.

Kwenye sehemu ya maelezo ya chapisho hilo, alitangaza kwa kejeli kwamba alikuwa katika maduka ya Garden City na kubainisha kwamba alikuwa tayari kusikiliza ushauri.

“Habari ya asubuhi Kenya, ninaripoti moja kwa moja kutoka Garden City. Niko tayari kwa ushauri wako wa kuanza siku yangu, OG itaheshimiwa,” alisema.

Siku ya Jumatatu, mwimbaji huyo aliibu kwa kejeli baada ya kundi la wakosoaji kukejeli jumba la kifahari ambalo alimalizia kulijenga hivi majuzi.

Katika siku mbili zilizopita, wakosoaji kwenye mitandao ya kijamii wamekuwa wakikejeli jumba kubwa la kifahari ambalo rapa huyo alijenga huku wengine wakilinganisha na jumba la mall.

Katika majibu yake, Khaligraph alionekana kuwacheka wakosoaji hao huku akibainisha kwamba hayo ndiyo aina ya matatizo aliyoyataka.

"Unaamka unapata unatrend sababu umejenga nyumba kubwa inakaa kama maduka, Mungu anajua haya ndio matatizo niliyokuwa natamani," Khaligraph alisema.

Rapa huyo mahiri amekuwa akitrend haswa kwenye mtandao wa kijamii wa X asubuhi ya Jumatatu kwa sababu ya nyumba yake.

Picha ya Khaligraph na mama yake wakiwa wametulia ndani ya jumba hilo kubwa iliwekwa kwenye mtandao wa X  Jumapili jioni kabla ya mwanamtandao mmoja kuihariri na kuifanya kuonekana kama duka.

Wanamtandao wengine wengi walichukua picha iliyohaririwa na kuitumia kufanyia mzaha jumba hilo.




RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved