logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mjaka Mfine aomba radhi baada ya kushiriki kwa ‘challenge’ ya Mapangale

Mtengenezaji huyo wa maudhui ya mtandaoni alifanya challenge hiyo na Crazy Kennar

image
na Brandon Asiema

Mastaa wako22 November 2024 - 10:42

Muhtasari


  • Mjaka Mfine ameomba msamaha kwa wafuasi ambao alisema kuwa alisoma jumbe zao kwenye mtandao wake wa kijamii waliokashifu kuhusika kwake kwenye challenge ya mapangale.
  • Baadhi ya wakenya mtandaoni wamekashifu kushiriki kwake katika challenge hiyo, wakidai kuwa kushiriki kwake ni sawa na kuunga mkono visa vya mauaji ya wanawake.

caption

Mtengenezaji wa maudhui ya mtandaoni Mjaka Mfine ameomba radhi kwa wafuasi wake baada ya video aliyofanya ya challenge ya wimbo unaotambaa mtandaoni mapangale na Crazy Kennar kusambaa mtandaoni.

Baadhi ya wakenya mtandaoni wamekashifu kushiriki kwake katika challenge hiyo, wakidai kuwa kushiriki kwake ni sawa na kuunga mkono visa vya mauaji ya wanawake ambavyo vimekithiri nchini katika muda wa miezi mitatu iliyopita.

Aidha katika video aliyochapisha kwenye akaunti yake ya tik tok, Mjaka Mfine ameelezea kuomba radhi kwa wafuasi wake walioonekana kukwera naye kufanya challenge hiyo.

“Niko hapa kuomba msamaha… juzi nimefanya video na Crazy Kennar ya mapangale. Nilifanya challenge hiyo kwa sababu niliona ikiwa challenge sikuwa najua itashika watu wengi.” Alisema Mjaka Mfine

Kwa mujibu wake, Mjaka Mfine amesema kuwa alikuwa baadhi ya wanawake wa kwanza kabisa kuunda video ya kukashifu visa vya mauaji ya wanawake kupitia kaziyake ya kutengeneza maudhui.

“Hivi maajuzi nilitengeneza video kuhusu mauaji ya wanawake, nilikuwa mmoja wa watengenezaji maudhui wa kwanza kuongelelea jinsi wanwake wanauliwa tukitaka visa hivyo kusitishwa.” Aliongeza kusema Mjaka Mfine.

Mjaka Mfine ameomba msamaha kwa wafuasi ambao alisema kuwa alisoma jumbe zao kwenye mtandao wake wa kijamii waliokashifu kuhusika kwake kwenye challenge ya mapangale.

Mjaka Mfine amesisitiza kuwa hakufanya challenge hiyo kwa malengo ya kuunga mkono mauaji ya wanawake. Vile vile amesema kuwa amefuta video za challenge hizo alizochapisha mtandaoni akisema kuwa ameelewa alichokifanya.


Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved