logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchekeshaji Mulamwah aweka wazi vyanzo vyake vya mapato

Mulamwah anamiliki zaidi ya piki piki 40 zinazofanya biashara ya boda boda mjini Kitale

image
na Brandon Asiema

Mastaa wako10 January 2025 - 10:51

Muhtasari


  • Mulamwah amesema kuwa utajiri alionao unatokana na biashara zake mabli mbali ikiwemo biashara ya boda boda.
  • Mvcheshaji huyo amekuwa akijibu madai ya kuwa anadaiwa na mikopo ya mamilioni ya fedha.


Mtengenezaji wa maudhui ya mtandaoni David Oyando Omusi maaruud kama Mulamwah ameweka wazi vyanzo vyake vya mapato ili katika hatua ya kuwajibu watu wanaodai kuwa ametumbukia katika dimbwi la madeni.

Katika ujumbe kupitia ukurasa wake wa Instagram mnamo Alhamisi, mchekeshai huyo amabye pia ni mtengenezxaji wa maudhui ya mtandaoni alichapisha picha ya cheti cha umiliki wa gari yake aina ya Mercedes ambayo hivi maajuzi tetesi ziliienea mtandaoni kuwa lingetwaliwa kutokana na madeni.

Akijibu tetesi zinazosambaa mtandaoni, Mulamwah amesema kuwa ana vyanzo vingi vya kumpa mapato akiongeza kuwa picha anazochapisha mtandaoni kuhusu mtindo wa maisha yake ni kuwatia moyo watu wengine na wala si kujipendekeza.

Mulamwah amesema kuwa utajiri alionao unatokana na biashara zake mabli mbali ikiwemo biashara ya boda boda zaidi ya 40 ambazo ameajiri vijana katika mji wa Kitale kaunti ya Trans Nzoia.

Mbali na kumiliki pikipiki, mchekeshaji huyo pia amesema mapato yake yanatokana na akaunti ya Youtube, kuwa na Zaidi ya skiza tunes 100, uigizaji, usanii wa sauti, kazi ya redio, ushereheshaji, ukulima, uchekeshaji, maudhui ya mtandaoni, mauzo na mahusiano ya kimataifa.

Hata hivyo, Mulamwaha amewatajka wakosoaji wake kufahamu kuwa kila kitu kinawezekana na wajifunze kuwahongera wengine kutokana na juhudi na bidi zao.

“Tujifunze kuthamini juhudi za kila mtu na kusherehekea mafanikio yao. Daima kujivunia hatua zako ndogo maishani. Hatuchapishi ili kujionyesha, hatushindani - tunachapisha ili kuonyesha kwamba hali zinaweza kubadilika kila wakati na kwamba unaweza kutoka chochote hadi kitu fulani.” Aliandika Mulamwah kwenye ukurasa wake wa Instagram.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved