logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Usuli na safari ya wasanii Radio and Weseal kutoka Uganda

Radio and Weasel lilikuwa ni kundi la wanamziki wawili kutoka taifa la Uganda walioimba miziki chini ya Bendi maarufu ‘’Goodlyfe Crew’’

image
na Evans Omoto

Mastaa wako14 March 2025 - 16:58

Muhtasari


  • Msanii Moses Nakintije Sekibogo alimaarufu(Radio) na mwenzake Douglas Mayanja alimaarufu( Weasel) ni wasanii waliotamba na kuvuma sana miaka ya hapo awali ya  2008-2018.
  • Msanii Radio alikuwa maarufu na mpevu wa kuimba muziki aina ya  RnB ilihali  Weasel  Naye akitia na kuongezea utamu wake wa aina ya muziki wa Reggae Ragga iliyokuwa na msisimko wa kucheza na kukatika katika mtindo wake wa kipekee.

Safari na Usuli wa wasanii Radio and Weasel

Radio and Weasel lilikuwa ni kundi la wanamziki wawili kutoka taifa la Uganda walioimba miziki chini ya Bendi maarufu ‘’Goodlyfe Crew’’

Msanii Moses Nakintije Sekibogo alimaarufu(Radio) na mwenzake Douglas Mayanja alimaarufu( Weasel) ni wasanii waliotamba na kuvuma sana miaka ya hapo awali ya  2008-2018

Msanii Radio alikuwa maarufu na mpevu wa kuimba muziki aina ya  RnB ilihali  Weasel  Naye akitia na kuongezea utamu wake wa aina ya muziki wa Reggae Ragga iliyokuwa na msisimko wa kucheza na kukatika katika mtindo wake wa kipekee.

Moses Radio alianza tasinia yake ya mziki  akiwa shule ya upili kwanzia mwaka wa 1998 -2001 katika shule  upili ya msalaba mtakatifu  iliyoko Jinja ambapo kwa wakati huo pia alikuwa kiranja mkuu katika shule hiyo , akiwa shuleni aliweza kujiunga na klabu ya mashindano kwa Vijana ya mziki.

Akiwa pale shuleni Radio aliweza kukadiria mradi wa kubuni mradi kuhusu mziki ambapo ulielezea wazi faida za vipaji katika ulingo wa sanaa ya mziki kwa ujumla wasilisho lake hilo liliweza kushinda katika  siku ya mashindano.

 Hatimaye Radio alijiunga na Chuo kikuu cha Kiira ambapo aliendeleza kipaji chake kwa miaka miwili hatimaya  aliazimia kujiunga na kundi la msaniii maarufu Jose Chameleon akiwa anamfanyia kazi nguli huyo Jose Chameleon kama mtu wake wa mkono  aliweza kupewa fursa ya kuonyesha makali ya kipaji chake.

Aliweza kucharaza vibao kama  Jenniffer, Dagala, Wololo, na kibao chake Sweet Lady kibao ambacho kiliweza kuvuma na kupokelewa na mashabiki wake na kumtukuza na kumsifu kama msanii mchanga ambaye alikuwa amekuja kwa moto kama wa kivu.

Kwa upande mwingine Douglas Mayanja alimarufu Weasel alianza kama msanii wa kujitegemea  aliyekuwa akiimba kama msanii wa  kujitegemea  chini ya ulezi wa ndugu yake mkubwa, hatimaye Weasel alipata fursa ya kuimba kolabo kali sana na msanii Jose chameone  na wakacharaza kibao kimoja kiitwacho  ‘’ BOMBOCLAT’’ kibao ambacho kilivuma sana.

Baadhi ya vibao ambavyo wasanii hawa waliweza kuvicharaza ni kama Nakudata mwaka wa 2008,Lwaki Onumya,Zuena,Nyambura na kibao cha Bread and Butter.

Wasanii hawa waliweza kupokea zawadi nyingi katika taasinia yao hio ya muziki na kupata tuzo kibao kama tuzo ya Mziki wa  HIPpop 2015,Hipipo wimbo bora wa mwaka 2015, Peal  African music Award wimbo bora wa mwaka Nakudata  2008 miongoni mwa tuzo nyingine nyingi.

Mnamo mwaka wa 2018 msanii Radio Aliaga dunia  kutokana na majeraha ya akili baada ya kupigwa na mlinzi wa usalama katika klabu moja kule Entebee alipokuwa akiwasilisha na kuimba katika klabu na kutupwa mita tatu kutoka juu na kurushwa chini sakafuni ambapo alipata majeraha kadhaa yaliomsababishia mauti yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved