logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Willy Paul apanda bei, afichua ada zake mpya za juu

Ili kutumbuiza katika klabu iliyo jijini Nairobi, Willy Paul  sasa anatoza ada ya Ksh 600,000.

image
na Radio Jambo

Habari12 November 2022 - 12:14

Muhtasari


•Mapromota watakaomtaka aonekane tu kwenye klabu bila kutumbuiza watalazimika kulipa Sh300,000.

•Wamiliki wa makampuni watalazimika kumlipa shilingi milioni 30  ili kuwa balozi wa bidhaa zao.

Mwimbaji Wilson Radido almaarufu Willy Paul ameobgeza  ada ya huduma zake.

Siku ya Jumamosi, mwimbaji huyo wa nyimbo za injili wa zamani alifichua kadi yake mpya ya kazi  iliyo na ada mpya za aina tofauti za huduma anazotoa.

"Kadi yangu ya bei iliyosasishwa" aliandika kwenye Instagram.

Kulingana na kadi hiyo mpya, mapromota watakaomtaka aonekane tu kwenye klabu bila kutumbuiza watalazimika kulipa Sh300,000.

Ili kutumbuiza katika klabu iliyo jijini Nairobi, Willy Paul  sasa anatoza ada ya Ksh 600,000.

Itagharimu Ksh 200,000 kuweka tangazo moja kwenye Instastori za mwimbaji huyo. Kufanya matangazo kwenye ukurasa wake wa Instagram  itagharimu shilingi nusu millioni kwa kila chapisho.

Wamiliki wa makampuni watalazimika kumlipa shilingi milioni 30  ili kuwa balozi wa bidhaa zao.

Willy Paul pia anatoza Ksh shilingi milioni moja unusu ili kutumbuiza katika hafla yoyote ya nje. Wanaohitaji huduma zake wameagizwa kuwasiliana naye kupitia [email protected].

Haya yanajiri siku chache tu baada ya msanii huyo aliyezingirwa na utata mwingi kujigamba kuhusu umahiri wake unaomfanya awe na kiburi.

Willy Paul alisema  kuwa yeye hajali watu wanasema nini kwani hakuna anayempatia chakula wala kitu chochote.

 "Si hakuna mtu ananilisha? Alafu si niko na pesa na maisha fiti alafu mimi ni  Mluo mzuri! " Alijigamba Willy Paul.

Aliendelea kuwachana wasanii wenzake kwa kudai kuwa hakuna anayekaribia kiwango chake, hivyo sababu nyingine ya yeye kujivunia.

Zaidi ya hayo, mimi ndiye mwanamuziki mahiri zaidi hapa Kenya.... Baaass!" alisema Pozze.

Wiki chache zilizopita mwimbaji huyo alionyesha magari yake katika kile kilichoonekana kama jibu kwa wakosoaji wake. Hapo awali alizindua Mercedes Benz mpya ya rangi ya majano.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved