logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Anaendelea vyema,' Raila amtembelea seneta wa Garissa Yusuf Haji

"Nilimtembelea seneta wa Garissa Yusu Haji, mwenyekiti wa kamati ya BBI

image
na Radio Jambo

Burudani15 October 2020 - 15:31

Muhtasari


  • Seneta Yusuf Haji alianguka nyumbani kwake na kufanyiwa upasuaji 
  • Kinara wa ODM Raila Odinga amtembelea nyumbani kwake.

Seneta wa Garissa Yusuf Haji anaendelea vyema hii ni baada ya kuanguka nyumbani kwake na kufanyiwa upasuaji wa dharura wiki chache zilizopita.

Kupitia ukurasa wake wa twitter kinara wa ODM Raila Odinga aliweka picha na kuandika ujumbe kuwa seneta huyo anaendelea vyema baada ya upasuaji huo.

"Nilimtembelea seneta wa Garissa Yusu Haji, mwenyekiti wa jopo la BBI, seneta anaendelea vyema nyumbani kwake  baada ya kulazwa hospitalini tunamtakia afueni ya haraka." Aliandika Raila.

 
 

Raila alikuwa ameandamana na kiranja wa wachache  katika bunge ambaye pia ni mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohammed aliyesema kuwa walizungumzia mambo ya serikali.

"Niliandamana na kiongozi wangu wa ODM kumtembelea seneta Yusuf Haji ambaye anaendelea vyema nyumbani kwake alikuwa mchangamfu. tulizungumzia mambo muhimu ya serikali."

Seneta huyo alianguka akiwa nyumbani kwake mnamo tarehe 29 Septemba mwaka huu.

(Mhariri Davis Ojiambo)

 

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved