- Seneta Yusuf Haji alianguka nyumbani kwake na kufanyiwa upasuaji
- Kinara wa ODM Raila Odinga amtembelea nyumbani kwake.
Seneta wa Garissa Yusuf Haji anaendelea vyema hii ni baada ya kuanguka nyumbani kwake na kufanyiwa upasuaji wa dharura wiki chache zilizopita.
Kupitia ukurasa wake wa twitter kinara wa ODM Raila Odinga aliweka picha na kuandika ujumbe kuwa seneta huyo anaendelea vyema baada ya upasuaji huo.
Visited Garissa Senator Yusuf Haji, the chairman of the Steering Committee on the Implementation of the Building Bridges to a United Kenya Taskforce Report. Senator is recuperating at home following recent hospitalization. We wish him a full and speedy recovery. pic.twitter.com/9b4OMZxWnQ
— Raila Odinga (@RailaOdinga) October 15, 2020
"Nilimtembelea seneta wa Garissa Yusu Haji, mwenyekiti wa jopo la BBI, seneta anaendelea vyema nyumbani kwake baada ya kulazwa hospitalini tunamtakia afueni ya haraka." Aliandika Raila.
Raila alikuwa ameandamana na kiranja wa wachache katika bunge ambaye pia ni mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohammed aliyesema kuwa walizungumzia mambo ya serikali.
"Niliandamana na kiongozi wangu wa ODM kumtembelea seneta Yusuf Haji ambaye anaendelea vyema nyumbani kwake alikuwa mchangamfu. tulizungumzia mambo muhimu ya serikali."
Seneta huyo alianguka akiwa nyumbani kwake mnamo tarehe 29 Septemba mwaka huu.
(Mhariri Davis Ojiambo)