logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msiba wa kujitakia: Nilikubali kuwa mpenzi wa kaka wawili –Sasa wote wanataka kunioa

Maria anasema anatafuta muda bora wa kupasua mbarika

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 November 2020 - 15:05

Muhtasari


 

  •  Hizi sasa ni sakata za kujitakia 
  •  Maria anasema anatafuta muda bora wa kupasua mbarika 
  •  Anasema amewapenda kaka wawili 

 

Mwiba kujidunga hauambiwi pole . sasa waliotoa msemo huo walijua wanachosema  na ndio hali ambayo  Maria Khatuve anajipata .

 Alikosa msimamo wakati kaka wawili walipoanza kumtongoza na kwa sababu ya tamaa  anasema alianza kuoyesha ishara za kuwakubali wote huku kila mmoja akizidi  kumkaribia . sasa tatizo ni kwamba kaka hao  hawajui kwamba  Maria anazungumza na mwingine . Imefika wakati wote wawili  wanataka kumuoa . Maria ameshindwa atafanya nini kwa sababu alifikiri mwanzoni kwamba ni utani lakini anapofuatilia mambo ,anagundua kwamba kaka  hao wanataka kufanya harusi yao kwa pamoja ,siku moja na wameshaambiana kuhusu uhusiano wao na mwanamke wanayempenda bila kujua kwamba ni mwanamke mmoja .

 Maria amekuwa  na woga wa kuwaambia kaka hao kwamba alifanya kosa kwa kuedelea kuzungumza  nao na kuwapa wote matumaini kwamba amewakubali katika uhusiano ambao sasa umepiga takriban miaka miwili . Aliwajua wakati mmoja na kila mmoja akachukua nambari yake ingawaje wakati tofauti na  hapo ndipo ngoma hiyo ilipoanzia .

 Maria anasema mwanzoni alifikiri kaka hao walikuwa wanajua wanachofanya kwani  jumbe zao na hata mazungumzo kati yake nao yalikuwa yakifanyika  wakati sawa na akajua wanamchezea shere lakini baadaye aligundua kwamba walikuwa wanaishi miji mbali mbali na hivyo basi hawakujua kwamba wanazungumza na mwanamke mmoja .

 Amekutana nao kwa deti  lakini kamwe hakuthibutu kujisema akihofia kwamba huenda angewatenganisha au kuwapoteza wote . lengo lake anasema lilikuwa kutumia muda mrefu kadri ya uwezo wake kumtambua aliye bora kati yao kisha kumueleza mwingine kuhusu kinachofanyika lakini amejipata kuwapenda wote kwa njia sawa kwani kila mmoja na sifa zake nzuri na udhaifu wake . Maria sasa amekanganywa na kaka hao wa familia moja lakini kwa sababu kila mmoja  amepiga hatua ya kutaka kuwasilisha posa anajua wakati umewadia kwa kusema ukweli lakini bado anaogopa matokeo ya hatua yake ya kusema ukweli .

  

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved