logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majambazi watano wapigwa risasi Kakamega

Bunduki mbili na mavazi ya polisi ni baadhi ya vitu vilivyopatikana kwenye tukio hilo

image
na Radio Jambo

Habari19 May 2021 - 06:28

Muhtasari


•Watano hao walikataa kutii amri ya kusimama na wakaanza kupiga risasi

•Bunduki mbili na mavazi ya polisi ni baadhi ya vitu vilivyopatikana kwenye tukio hilo

Crime scene

Majambazi watano waliuliwa kwa kupigwa risasi alasiri ya Jumanne katika eneo la Makhokho lilio kwenye barabara ya  Kakamega-Kisumu.

Watano wale walikabiliwa na maafisa wa huduma maalum(SSP) walipokuwa wanatoka kwenye shughuli yao ya wizi wa kimabavu mjini Kakamega.

Maafisa wa SSP walilazimishwa kutumia bunduki zao baada ya watano wale waliokuwa wanasafiri kwa gari ndogo aina ya Toyota Belta kupuuza amri ya kusimama na kisha kuanza kupiga marisasi kuelekeza upande waliokuwa maafisa wale.

Hata hivyo, mashambulio ya majambazi wale waliokuwa wamejihami kabisa hayafua dafu kwani maafisa wa SSP waliwapiku nguvu na kuwaacha katika hali mahututi.

Shirika la kuchunguza uhalifu(DCI) lilitangaza kuwa watano wale walikuwa wanapanga njama ya kutekelea uhalifu mjini Bungoma na Mumias.

Bunduki mbili zilizokuwa na risasi, simu ya polisi na mavazi ya polisi ni baadhi ya bidhaa zilizopatikana na majambazi wale.

Bidhaa zilizopatikana

Hakuna yeyote kati yao aliyenusurika huku miili yao ikihifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Kakamega County Referral Hospital.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved