logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mutyambai awapongeza polisi kwa kuzingatia nidhamu kwenye uchaguzi

Inspekta mkuu wa polisi aliwaahidi Wakenya kuwa kesi ndogondogo zilizoripotiwa  zitashughulikiwa ifaavyo na watakaopatikana na hatia kupelekwa kotini

image
na Radio Jambo

Makala20 May 2021 - 05:13

Muhtasari


•Inspekta mkuu wa polisi pia aliwapongeza wanahabari, IEBC na wakaazi wa maeneo ya Juja, Bonchari na Rurii

• Ripoti nyingi za utumizi mbaya wa wanapolisi ziliripotiwa maeneo ya Juja na Bonchari

Mutyambai

Mkaguzi mkuu wa polisi nchini Kenya, Hillary Mutyambai amepongeza wakaazi maeneo bunge ya Bonchari na Juja na wadi ya Rurii kwa kushiriki uchaguzi wenye amani katika uchaguzi mdogo uliofanyika katika maeneo hayo.

Kwa kuongezea, Mutyambai amewapongeza maafisa wa polisi kwa kulinda amani na haki wakizingatia nidhamu na heshima.

 “Nawaahidi Wakenya kuwa kesi ndogondogo zilizoripotiwa kwa wanapolisi zitashughulikiwa ifaavyo na watakaopatikana na hatia watapelekwa kotini” Mutyambai alisema.

Mkuu huyo wa polisi pia alipongeza tume ya IEBC , wanahabari na maafisa wote wa uchaguzi walioshirikiana pamoja hatua kwa hatua kwa maelewano.

Mutyambai alikuwa akizungumza  kupitia ujumbe uliotolewa kwa wanahabari siku ya Jumanne.

Hata hivyo, kulijitongeza ripoti nyingi za utumizi mbaya wa wanapolisi huku kiongozi wa ODM akikashifu kitendo hicho kwa ukali.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved