logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbona usiyafanye sasa hivi?- Junet akosoa ahadi za Ruto

Alisema kuwa lengo kuu la chama cha ODM  iwapo watatwaa uongozi ni kuimarisha uchumi wa Kenya na kuleta pesa mifukoni mwa Wananchi

image
na Radio Jambo

Burudani21 July 2021 - 05:33

Muhtasari


•Alipokuwa anahutubia wakazi wa Tana River mapema wiki hii, mbunge huyo wa Suna Mashariki aliwaomba Wakenya kutokubali viongozi ambao wanatoa ahadi ya kesho ilhali wana uwezo wa kuyatimiza kwa sasa.

•Mbunge huyo pia alikosoa mpango wa wanasiasa wanaounga naibu rais mkono wa kupatia vijana toroli akidai kuwa hazisaidii kutatua shida za Wakenya. Alisema kuwa siasa zao ni za kuwahadaa Wakenya.

JUNET.jfif

Kiongozi wa walio wachache bungeni Junet Mohamed ametia doa kampeni za naibu rais William Ruto za kuwania urais mwaka ujao akisema kuwa anawapa Wakenya ahadi anazoweza kutimiza kwa sasa.

Junet amepuuzilia mbali ahadi ambazo Ruto anawapa Wakenya akidai kuwa iwapo kweli ana nia  yuko katika nafasi  ya kutimiza anayoyahidi kwa sasa kuona kuwa yuko serikalini tayari.

Alipokuwa anahutubia wakazi wa Tana River mapema wiki hii, mbunge huyo wa Suna Mashariki aliwaomba Wakenya kutokubali viongozi ambao wanatoa ahadi ya kesho ilhali wana uwezo wa kuyatimiza kwa sasa.

"Watu ambao wako ndani ya serikali wanakuja hapa na kuwaambia eti ukinichagua nitakufanyia hii na hii na hii. Swali ambalo mnafaa muwaulize ni mbona usifanye hayo saa hizi? Si uko serikalini? Mbona unangoja tukuchague ndio ufanye?.. ni lazima mtu afanye kile anachoweza kwa sasa"  Junet alisema.

Mbunge huyo pia alikosoa mpango wa wanasiasa wanaounga naibu rais mkono wa kupatia vijana toroli akidai kuwa hazisaidii kutatua shida za Wakenya. Alisema kuwa siasa zao ni za kuwahadaa Wakenya.

"Wanatembea na pesa ambayo wamepora ndio wanataka kununua nayo wananchi. Wanakuja hapa na mambo ya Wheelbarrow ambayo hayawezi kusaidia Wakenya" Alidai Junet.

Alisema kuwa lengo kuu la chama cha ODM  iwapo watatwaa uongozi ni kuimarisha uchumi wa Kenya na kuleta pesa mifukoni mwa Wananchi.

"Sisi kama ODM tumejipanga na tunajua mwelekeo wetu. Lakini wale watu ambao wanakuja hapa kudanganya wananchi wakitumia umaskini kama silaha na kuwaambia lazima ubaki maskini ubaki hustler ndo akusaidie ni watu amabo wanakuja kuharibu uchumi wa Kenya. Lazima tujitenge na wao tubaki ODM" Junet alisema. 

Junet alitupilia mbali mfumo wa uchumi wa 'bottom up' ambao naibu rais anaahidi Wakenya na kusema kuwa mfumo wa ODM ikiongozwa na Raila Odinga  ni bora.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved