logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nadia Mukami kusajili msanii mpya

Msanii wa kike Nadia Mukami amesema kwamba atakuwa anatambulisha kwa umma msanii wake wa kwanza chini ya lebo ya Sevens Creative hub, mnamo tarehe 1/02/2022.

image
na Radio Jambo

Makala27 January 2022 - 07:26

Muhtasari


• Msanii wa kike Nadia Mukami amesema kwamba atakuwa anatambulisha kwa umma msanii wake wa kwanza chini ya lebo ya Sevens Creative hub, mnamo tarehe 1/02/2022.

• Kabla ya hapo atakuwa anafanya collabo na msanii huyo wiki kesho huku wengi wakisubiri kushuhudia kipaji hicho.

• Mpaka sasa haijafahamika iwapo chipukizi huyo atakuwa ni wa kiume ama wa kike, ikimaanisha kwamba italazimu mashabiki kusubiri hadi tarehe ya uzinduzi.

Msanii wa kike Nadia Mukami amesema kwamba atakuwa anatambulisha kwa umma msanii wake wa kwanza chini ya lebo ya Sevens Creative hub, mnamo tarehe 1/02/2022.

Kabla ya hapo atakuwa anafanya collabo na msanii huyo wiki kesho huku wengi wakisubiri kushuhudia kipaji hicho.

Mpaka sasa haijafahamika iwapo chipukizi huyo atakuwa ni wa kiume ama wa kike, ikimaanisha kwamba italazimu mashabiki kusubiri hadi tarehe ya uzinduzi.

Swala kuu katika mchakato huu mzima, ni kupata maelezo kamili kuhusu urefu wa mkataba baina ya Sevens Creative hub na chipukizi huyo na mazingira ya kazi yatakuwa na sheria gani na pia msanii mwenyewe atakuwa na mikakati gani ya kustahimili uzito wa sanaa ya muziki hapa Kenya.

Lebo nyingi kwa kipindi Cha nyuma wamekuwa wakitofautiana na usimamizi wao kwa sababu ya hela, mashabiki wengi wakiamini kuwa mara hii hakutakuwa na mtafaruku huo ,ikifahamika kuwa Mukami alishawahi kupitia matatizo hayo na lebo tofauti na akajifunza kwayo.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved