logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mrembo aliyefunga ndoa na mdoli wa viraka amuacha kwa kuchepuka na kumng'oa uume

Alisema: 'Niligundua wakati rafiki yangu alinitumia ujumbe jioni moja akisema kwamba alikuwa akinisaliti.

image
na Davis Ojiambo

Habari07 June 2023 - 13:52

Muhtasari


  • • Alisema: 'Niligundua wakati rafiki yangu alinitumia ujumbe jioni moja akisema kwamba alikuwa akinisaliti."
  • • Aliongeza: "Ni mpira mweupe, ambao una urefu wa 16cm. Kwa hivyo niliamua kuiondoa. Nimeifanya hapo awali."
Meirivone Rocha Moraes, mrembo aliyefunga ndoa na mdoli wa viraka asema alichepuka.

Mwanamke aliyegonga vichwa vya habari nchini Brazili baada ya 'kuolewa' na mdoli wa viraka ambaye mama yake alimtengenezea anadai kuwa mpenzi wake amemsaliti kimapenzi kwa mara nyingine.

Meirivone Rocha Moraes, kutoka Brazili, amejulikana sana katika miaka michache iliyopita kwa kushiriki mambo ya ndani na nje yake na uhusiano wa kitu kisicho hai.

Kufuatia madai ya kusalitiwa kimapenzi, msichana huyo mwenye umri wa miaka 37 anasema mdoli huyo wa mapenzi kwa sasa analala kwenye sofa na hata akamnyang’anya ‘uume’ wake.

Alisema: 'Niligundua wakati rafiki yangu alinitumia ujumbe jioni moja akisema kwamba alikuwa akinisaliti. Kwa hiyo usiku huo, nilipatwa na hali mbaya sana na kumfanya alale kwenye kochi.'

Na kama adhabu yake, Meirivone, aliamua kutenganisha uume wa Marcelo.

Aliongeza: "Ni mpira mweupe, ambao una urefu wa 16cm. Kwa hivyo niliamua kuiondoa. Nimeifanya hapo awali.

'Ninaogopa wanawake wengine watagusa uume wa Marcelo kwa hivyo napenda kuuweka kwenye droo ya [chupi] tunapotoka kwenda kwenye baa au maonyesho.

'Basi, hakuna nafasi ya wanawake wengine kumtamani.'

Marcelo anadaiwa kumsaliti Meirivone siku za nyuma.

Alisema: 'Mara ya mwisho, nilipata uzi wa waridi nyangavu kwenye sakafu.

 

'Niligundua kuwa Marcelo alikuwa na mwanamke mwingine lakini nilipomuuliza ni akina nani, hakunijibu.

'Marcelo ni mtukutu, anawafuata wanawake kisha ananidanganya kuwa hakuna kinachotokea.'

 

Pia anadai kuwa mwanasesere huyo ana mawasiliano zaidi ya 500 kwenye WhatsApp yake, wote wakiwa ni wanawake.

 

Aliongeza: 'Kila mara ninamshika katika mazungumzo na msichana, na ninapouliza ni nani, anajaribu kusema ni binamu yake.'

 

Kwa sasa, Marcelo anaendelea kulala kwenye sofa, na bado hajapokea uume wake, jarida la nchini humo liliripoti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved