logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baba mkwe agundua kijana anayemuoa bintiye ana sura mbaya, ataka harusi kusitishwa

Tukio hilo lisilo la kawaida lilizua mvutano mkali wa mawazo.

image
na Davis Ojiambo

Habari09 August 2023 - 08:14

Muhtasari


  • • Unahisi ni sahihi kwa mtu, haswa mrembo kuzingatia jinsi mpenzi wake anavyoonekana kabla ya kuingia katika ndoa naye?
Kuvunjika kwa uume kunaweza kutokea kwa sababu ya kubadilisha mitindo ya kujamiana wakati wa kushiriki tendo la ndoa.

Harusi moja ililazimika kustishwa ghafla baada ya baba mkwe kudaiwa kutoa agizo hilo alipogundua kwamba kijana aliyepanga kufunga harusi na binti yake ana sura mbaya.

Kwa mujibu taarifa hiyo iliyogeuka kuwa mada ya mjadala katika kituo kimoja nchini Tanzania, babamkwe huyo ambaye hakutambuliwa kwa jina alifika katika siku kubwa ya binti yake lakini inaarifiwa baada ya kumuona mkwe mtarajiwa, hakupendezwa na sura yake.

Hapo ndipo mzee alijongea nyuma na kuwataka waandalizi wa hafla ya harusi kuipiga breki mara moja akisema kwamba hakuipenda sura ya bwana harusi ambaye alikuwa mkwe wake mtarajiwa.

Tukio hilo lisilo la kawaida lilizua mvutano mkali wa mawazo kutoka kwa watangazaji na watu waliochangia mada yenyewe.

Baadhi ya wanawake walisema kuwa sura au muonekano wa mwanaume wa kuzaa naye inazingatiwa sana, kando na elimu na utajiri ambavyo kwa muda mrefu vimekuwa vikichukuliwa kama kigezo muhimu cha mwanamke anapomchagua mwanamume wa kuolewa naye.

Kwa upande wa wanaume, wengi walionekana kuchoshwa na vigezo vingi ambavyo wanawake wanawawekea kutoka utajiri, umbo la iraba minne, urefu, rangi ya ngozi ya hudhurungi na sasa sura pia.

Wengine pia walimsuta baba mkwe kwa kuingilia kati suala la mapenzi ya bintiye, kwani tayari alikuwa ameshamubali mkaka wa watu na sura hiyo ambayo baba aliikataa kuwa haina mshiko.

“Cha kwanza kwa mwanamume ni Amani, nafsi inasema nini kwako, ndio maana unaweza kupita barabarani ukamuona mtu kilema, kipofu au upungufu Fulani lakini ana mtu. Kwa mwanaume kinachokuwa na maana Zaidi ni Amani wala si sura. Mpaka anakupeleka kukutambulisha kwao mana yake ameshakubali kwamba hapa ndio tulizo langu la Amani liko,” mmoja alisema.

“Wanawake wakati mwingine wanataka vitu vingi sana, kuna muda watahitaji gym mtu wa miraba minne, kuna muda wanahitaji mtu wa ndevu, kuna muda wanahitaji mtu mrefu, mtu mwenye pesa,” mwingine alisema.

Unahisi ni sahihi kwa mtu, haswa mrembo kuzingatia jinsi mpenzi wake anavyoonekana kabla ya kuingia katika ndoa naye?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved