logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto akiri kukubiliana na Raila walipokutana na Museveni nchini Uganda

Ruto amekariri uamuzi kumuunga mkono Raila kuwa mwenyekiti wa AUC.

image
na Davis Ojiambo

Habari27 February 2024 - 13:29

Muhtasari


  • Alisisitiza kuwa hakuna Mkenya anayefaa kutengwa na serikali licha ya matokeo ya kura.
  •  
  • Rais William Ruto ameelezea uamuzi wake wa kumuunga mkono aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kwa wadhifa wa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika kwa .

Rais William Ruto amekariri msimamo wake kumuunga mkono aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kwa wadhifa wa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika kwa mara ya kwanza tangu wawili hao wakutane nchini Uganda Jumatatu, Februari 26.

Akiongea wakati wa Kongamano la Uwekezaji katika Kaunti ya Homa Bay mnamo Jumanne, Februari 27, Ruto aliwakumbusha wakaazi kwamba kila mara amekuwa akitayarisha mpango wa kuunganisha taifa baada ya uchaguzi wa urais wa 2027 uliokumbwa na utata.

Alisisitiza kuwa hakuna Mkenya anayefaa kutengwa na serikali licha ya matokeo ya kura.

Mkataba huo uliafikiwa nchini Uganda huku wawili hao wakiwa wenyeji wa Rais Yoweri Museveni.

"Nilikuwa hapa Homa Bay wakati wa kampeni na niliwaahidi kuwa hakuna atakayeshindwa hapa Kenya, niliahidi kwamba nitajitahidi sana kuhakikisha kila mtu anapata nafasi, hamkuniamini, sasa mnaona. Mambo yanaendaje.Si niliahidi hilo sokoni?

"Kuna nafasi kwa ajili yetu sote. Hushindi kwa kuwafanya wengine washindwe. Tunataka hali ya ushindi kwa Wakenya wote. Hakuna Wakenya walio katika upinzani na walio serikalini,"  rais alieleza.

Hii ilikuwa mara ya kwanza  Ruto kutoa maoni yake kuhusu azma ya Raila kuwania uwenyekiti wa tume ya umoja wa Afrika (AUC). Raila, mnamo  siku ya Jumatatu, aliwasifu Ruto na Museveni kwa kuunga mkono ombi lake, na wakati huo huo akamtambua hasimu wake kisiasa kama Rais wa Kenya.

"La muhimu zaidi, kwa kuhimizwa na Rais Museveni, tulijadili pia juu ya kugombea kwangu uwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika. Ninamshukuru sana Rais Museveni kwa kuniuga mkono na kwa Rais Ruto kwa kuniunga mkono kikamilifu," Raila alieleza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved