logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanawake wawili wauawa kinyama na mshukiwa wa wizi Meru

Naibu wa chifu wa alikashifu mauaji hayo na kuhakikishia umma kuwa utawala wake utahakikisha muuaji huyo ameadhibiwa.

image
na

Habari17 April 2024 - 05:17

Muhtasari


• Miili hiyo ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Kanyakine.

Polisi na wakaazi katika eneo ambapo miili ya wanawake wawili waliouawa katika eneo la Kiigene huko Nkubu, kaunti ya Meru mnamo Aprili 16, 2024. Picha: GERALD MUTETHIA

Wanawake wawili wenye umri wa kati ya miaka 25-30 waliuawa Jumanne asubuhi na mshukiwa wa wizi wa mbao eneo la Kiigene huko Nkubu, Imenti Kusini, Meru.

Shahidi Muthomi Mburugu alisema kuwa marehemu walimuona mshukiwa akivamia karakana hiyo na kabla hawajapiga mayowe kuitisha msaada, mshukiwa aligundua kuwa walikuwa wamemwona ndipo akawavamia.

“Tumesikitishwa na mauaji ya kikatili ya wanawake wawili, tumeshtushwa sana kuwapoteza vijana wa aina hii, nilisikia mayowe barabarani lakini sikuweza kusaidia kwa wakati, niliona miili yao ikiwa imelala barabarani,” Mburugu alisema.

Mburugu alivitaka vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wa kina utakaofanikisha kukamatwa na kufikishwa mahakamani kwa mtuhumiwa huyo.

Msaidizi wa chifu wa Kiigine Joseph Muthuri alikashifu mauaji hayo na kuhakikishia umma kuwa utawala wake utahakikisha muuaji huyo ameadhibiwa.

"Wawili hao walikuwa na umri wa kati ya miaka 25-30. Mshukiwa aliyewaua alionekana na wanawake wawili waliofariki akivunja karakana ili kuiba. Tutahakikisha tunamkamata mshukiwa," Muthuri alisema.

"Natoa wito kwa majirani ambao wanaweza kuwa na taarifa muhimu zinazoweza kusababisha kukamatwa kwa watu hao washirikiane nasi kumpata mtuhumiwa," alisema.

Miili hiyo ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Kanyakine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved